Sura: SWAAD 

Aya : 59

هَٰذَا فَوۡجٞ مُّقۡتَحِمٞ مَّعَكُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِهِمۡۚ إِنَّهُمۡ صَالُواْ ٱلنَّارِ

Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni



Sura: SWAAD 

Aya : 60

قَالُواْ بَلۡ أَنتُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِكُمۡۖ أَنتُمۡ قَدَّمۡتُمُوهُ لَنَاۖ فَبِئۡسَ ٱلۡقَرَارُ

Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusababishia haya, napo ni pahala pabaya kabisa!



Sura: SWAAD 

Aya : 61

قَالُواْ رَبَّنَا مَن قَدَّمَ لَنَا هَٰذَا فَزِدۡهُ عَذَابٗا ضِعۡفٗا فِي ٱلنَّارِ

Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusababishia haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni



Sura: SWAAD 

Aya : 62

وَقَالُواْ مَا لَنَا لَا نَرَىٰ رِجَالٗا كُنَّا نَعُدُّهُم مِّنَ ٱلۡأَشۡرَارِ

Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahesabu ndio katika waovu?



Sura: SWAAD 

Aya : 63

أَتَّخَذۡنَٰهُمۡ سِخۡرِيًّا أَمۡ زَاغَتۡ عَنۡهُمُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ

Tulikosea tulipo wafanyia mas-khara, au macho yetu tu hayawaoni?



Sura: SWAAD 

Aya : 64

إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقّٞ تَخَاصُمُ أَهۡلِ ٱلنَّارِ

Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni



Sura: GHAAFIR 

Aya : 6

وَكَذَٰلِكَ حَقَّتۡ كَلِمَتُ رَبِّكَ عَلَى ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَنَّهُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِ

Namna hivi limewathibitikia makafiri neno la Mola wako Mlezi ya kwamba wao ni watu wa Motoni



Sura: GHAAFIR 

Aya : 46

ٱلنَّارُ يُعۡرَضُونَ عَلَيۡهَا غُدُوّٗا وَعَشِيّٗاۚ وَيَوۡمَ تَقُومُ ٱلسَّاعَةُ أَدۡخِلُوٓاْ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ أَشَدَّ ٱلۡعَذَابِ

Wanaonyeshwa Moto asubuhi na jioni. Na itakapofika Saa ya Kiyama patasemwa: Waingizeni watu wa Firauni katika adhabu kali kabisa!



Sura: GHAAFIR 

Aya : 47

وَإِذۡ يَتَحَآجُّونَ فِي ٱلنَّارِ فَيَقُولُ ٱلضُّعَفَـٰٓؤُاْ لِلَّذِينَ ٱسۡتَكۡبَرُوٓاْ إِنَّا كُنَّا لَكُمۡ تَبَعٗا فَهَلۡ أَنتُم مُّغۡنُونَ عَنَّا نَصِيبٗا مِّنَ ٱلنَّارِ

Na watakapo hojiana huko Motoni, wanyonge watawaambia walio jitukuza: Hakika sisi tulikuwa wafuasi wenu, basi je, hamtuondolei sehemu ya huu Moto?



Sura: GHAAFIR 

Aya : 48

قَالَ ٱلَّذِينَ ٱسۡتَكۡبَرُوٓاْ إِنَّا كُلّٞ فِيهَآ إِنَّ ٱللَّهَ قَدۡ حَكَمَ بَيۡنَ ٱلۡعِبَادِ

Watasema walio jitukuza: Hakika sote sisi tumo humo humo! Kwani Allah ameshahukumu baina ya waja!



Sura: AZZUKHRUF 

Aya : 74

إِنَّ ٱلۡمُجۡرِمِينَ فِي عَذَابِ جَهَنَّمَ خَٰلِدُونَ

Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannamu



Sura: AZZUKHRUF 

Aya : 75

لَا يُفَتَّرُ عَنۡهُمۡ وَهُمۡ فِيهِ مُبۡلِسُونَ

Hawatapumzishwa nayo, na humo watakata tamaa



Sura: AZZUKHRUF 

Aya : 76

وَمَا ظَلَمۡنَٰهُمۡ وَلَٰكِن كَانُواْ هُمُ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Wala Sisi hatukuwadhulumu, bali wao ndio walio kuwa madhalimu



Sura: QAAF 

Aya : 24

أَلۡقِيَا فِي جَهَنَّمَ كُلَّ كَفَّارٍ عَنِيدٖ

(Allaah Atasema): Mtupeni katika Jahannam kila kafiri, mkaidi!



Sura: QAAF 

Aya : 25

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٖ مُّرِيبٍ

Mzuiaji wa kheri, mwenye kuruka mipaka, mwenye kutia shaka



Sura: QAAF 

Aya : 26

ٱلَّذِي جَعَلَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَأَلۡقِيَاهُ فِي ٱلۡعَذَابِ ٱلشَّدِيدِ

Ambaye amefanya mwabudiwa mwengine pamoja na Allah, basi mtupeni katika adhabu kali



Sura: AL-QAMAR

Aya : 47

إِنَّ ٱلۡمُجۡرِمِينَ فِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٖ

Hakika wahalifu wamo katika upotofu na wazimu



Sura: AL-QAMAR

Aya : 48

يَوۡمَ يُسۡحَبُونَ فِي ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمۡ ذُوقُواْ مَسَّ سَقَرَ

Siku watakayoburutwa motoni kifudi fudi, Waambiwe: Onjeni mguso wa moto mkali mno



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 41

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni, je, ni wepi watu wa kushotoni?



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo



Sura: ALJINN 

Aya : 15

وَأَمَّا ٱلۡقَٰسِطُونَ فَكَانُواْ لِجَهَنَّمَ حَطَبٗا

Na ama wanaoacha haki, hao watakuwa kuni za Moto wa Jahannamu



Sura: ALJINN 

Aya : 23

إِلَّا بَلَٰغٗا مِّنَ ٱللَّهِ وَرِسَٰلَٰتِهِۦۚ وَمَن يَعۡصِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَإِنَّ لَهُۥ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدًا

Isipokuwa nifikishe Ujumbe utokao kwa Allah, na ujumbe wake. Na wenye kumuasi Allah na Mtume wake, basi hakika hao watapata Moto wa Jahannamu wadumu humo milele



Sura: ANNAAZIAAT 

Aya : 37

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

Basi yule aliyepindukia mipaka na kuasi



Sura: ANNAAZIAAT 

Aya : 38

وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Na akapenda zaidi maisha ya dunia



Sura: ANNAAZIAAT 

Aya : 39

فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!



Sura: AL-BURUJI 

Aya : 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 6

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمۡ شَرُّ ٱلۡبَرِيَّةِ

Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 8

وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 9

فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!



Sura: AL-QAARIAH 

Aya : 10

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ

Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?