Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 8

وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يَقُولُ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَبِٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَمَا هُم بِمُؤۡمِنِينَ

Na miongoni mwa watu wapo wanaosema[1] kuwa: “Tumemuamini Allah na Siku ya Mwisho” na[2] sio waumini (wa kweli)


1- - Kwa maneno tu.


2- - Ukweli ni kwamba…


Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 9

يُخَٰدِعُونَ ٱللَّهَ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَمَا يَخۡدَعُونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ

Wanamhadaa Allah na wale walioamini. Na hawahadai isipokuwa nafsi zao tu na wao hawatambui



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 10

فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ فَزَادَهُمُ ٱللَّهُ مَرَضٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡذِبُونَ

Ndani ya nyoyo zao kuna ugonjwa, na Allah akawaongezea ugonjwa. Na wanastahiki adhabu kali kwa uongo waliokuwa wanaufanya



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 11

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَا تُفۡسِدُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ قَالُوٓاْ إِنَّمَا نَحۡنُ مُصۡلِحُونَ

Na wanapoambiwa msifanye uharibifu ardhini wanasema: Hapana, bali sisi niwafanyaji mazuri



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 12

أَلَآ إِنَّهُمۡ هُمُ ٱلۡمُفۡسِدُونَ وَلَٰكِن لَّا يَشۡعُرُونَ

Elewa! Kwa yakini, wao ndio waharibifu hasa na lakini hawatambui



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 13

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ ءَامِنُواْ كَمَآ ءَامَنَ ٱلنَّاسُ قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ كَمَآ ءَامَنَ ٱلسُّفَهَآءُۗ أَلَآ إِنَّهُمۡ هُمُ ٱلسُّفَهَآءُ وَلَٰكِن لَّا يَعۡلَمُونَ

Na wanapoambiwa: Kuweni wenye kuamini kama walivyoamini watu, wanasema: Ah! Hivi tuamini kama walivyoamini wapumbavu? Elewa! Wao ndio wapumbavu hasa na lakini hawajui



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 14

وَإِذَا لَقُواْ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا وَإِذَا خَلَوۡاْ إِلَىٰ شَيَٰطِينِهِمۡ قَالُوٓاْ إِنَّا مَعَكُمۡ إِنَّمَا نَحۡنُ مُسۡتَهۡزِءُونَ

Na wanapokutana na walioamini wanasema: Tumeamini. Na wanapokuwa faragha na mashetani wao wanasema: Sisi tuko pamoja nanyi, tunachokifanya sisi tunacheza shere tu



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 15

ٱللَّهُ يَسۡتَهۡزِئُ بِهِمۡ وَيَمُدُّهُمۡ فِي طُغۡيَٰنِهِمۡ يَعۡمَهُونَ

Allah anawacheza shere wao, na anawapa muda zaidi katika kupotoka kwao huku wakiwa wanatangatanga



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 16

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ ٱشۡتَرَوُاْ ٱلضَّلَٰلَةَ بِٱلۡهُدَىٰ فَمَا رَبِحَت تِّجَٰرَتُهُمۡ وَمَا كَانُواْ مُهۡتَدِينَ

Hao ndio walioununua upotevu kwa uongofu. Biashara yao haikuleta faida, na hawakuwa waongofu



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 204

وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يُعۡجِبُكَ قَوۡلُهُۥ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَيُشۡهِدُ ٱللَّهَ عَلَىٰ مَا فِي قَلۡبِهِۦ وَهُوَ أَلَدُّ ٱلۡخِصَامِ

Na miongoni mwa watu wapo ambao zinakuvutia kauli zao katika maisha ya dunia, na wanamshuhudisha Allah juu ya yaliyo moyoni mwake hali yeye ni mpingaji mno



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 205

وَإِذَا تَوَلَّىٰ سَعَىٰ فِي ٱلۡأَرۡضِ لِيُفۡسِدَ فِيهَا وَيُهۡلِكَ ٱلۡحَرۡثَ وَٱلنَّسۡلَۚ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلۡفَسَادَ

Na anapoondoka (kwako) anahangaika huku na kule ardhini ili kufanya ufisadi humo na kuangamiza mimea na vizazi. Na Allah hapendi ufisadi



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 206

وَإِذَا قِيلَ لَهُ ٱتَّقِ ٱللَّهَ أَخَذَتۡهُ ٱلۡعِزَّةُ بِٱلۡإِثۡمِۚ فَحَسۡبُهُۥ جَهَنَّمُۖ وَلَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ

Na wanapoambiwa; Muogopeni Allah hupandwa na mori wa kufanya uovu. Basi kitakachowatosha ni Jahanamu na ni makazi mabaya mno



Sura: AL-IMRAN 

Aya : 167

وَلِيَعۡلَمَ ٱلَّذِينَ نَافَقُواْۚ وَقِيلَ لَهُمۡ تَعَالَوۡاْ قَٰتِلُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَوِ ٱدۡفَعُواْۖ قَالُواْ لَوۡ نَعۡلَمُ قِتَالٗا لَّٱتَّبَعۡنَٰكُمۡۗ هُمۡ لِلۡكُفۡرِ يَوۡمَئِذٍ أَقۡرَبُ مِنۡهُمۡ لِلۡإِيمَٰنِۚ يَقُولُونَ بِأَفۡوَٰهِهِم مَّا لَيۡسَ فِي قُلُوبِهِمۡۚ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يَكۡتُمُونَ

Na ili awapambanue wanafiki, na wakaambiwa: njooni mpigane katika njia ya Allah au lindeni. Wakasema: lau tungejua kuwa kuna mapigano bila ya shaka tungelikufuateni. wao siku ile walikuwa wako karibu zaidi na ukafiri kuliko imani, wanasema kwa midomo yao yasiyokuwemo nyoyoni mwao, na Allah ni mjuzi zaidi kwa yale wanayoyaficha



Sura: AL-IMRAN 

Aya : 168

ٱلَّذِينَ قَالُواْ لِإِخۡوَٰنِهِمۡ وَقَعَدُواْ لَوۡ أَطَاعُونَا مَا قُتِلُواْۗ قُلۡ فَٱدۡرَءُواْ عَنۡ أَنفُسِكُمُ ٱلۡمَوۡتَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Hao ndio ambao walisema kuhusu ndugu zao na wao wakiwa wamekaa: Lau wangelitutii sisi wasingeuliwa sema: basi ziondoleeni nafsi zenu kifo ikiwa nyinyi ni wa kweli



Sura: ANNISAI 

Aya : 60

أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ يَزۡعُمُونَ أَنَّهُمۡ ءَامَنُواْ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ وَمَآ أُنزِلَ مِن قَبۡلِكَ يُرِيدُونَ أَن يَتَحَاكَمُوٓاْ إِلَى ٱلطَّـٰغُوتِ وَقَدۡ أُمِرُوٓاْ أَن يَكۡفُرُواْ بِهِۦۖ وَيُرِيدُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَن يُضِلَّهُمۡ ضَلَٰلَۢا بَعِيدٗا

Je, hukuwaona wanaodai kuwa wameamini yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako wanataka wakahukumiane kwa Twaghuti[1], na ilhali wameamrishwa wamkatae? Na shetani anataka kuwapoteza upotevu wa mbali


1- - Twaghuti ni kila kinachoabudiwa na kutiiwa badala ya Allah ikiwa ni pamoja na shetani, sanamu, mzimu n.k.


Sura: ANNISAI 

Aya : 61

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ تَعَالَوۡاْ إِلَىٰ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ وَإِلَى ٱلرَّسُولِ رَأَيۡتَ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ يَصُدُّونَ عَنكَ صُدُودٗا

Na wanapoambiwa: Njooni kwenye yale aliyoyateremsha Allah na (njooni) kwa Mtume, utawaona wanafiki wanakuwekea pingamizi nyingi



Sura: ANNISAI 

Aya : 62

فَكَيۡفَ إِذَآ أَصَٰبَتۡهُم مُّصِيبَةُۢ بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيهِمۡ ثُمَّ جَآءُوكَ يَحۡلِفُونَ بِٱللَّهِ إِنۡ أَرَدۡنَآ إِلَّآ إِحۡسَٰنٗا وَتَوۡفِيقًا

Basi itakuwaje msiba utakapowafika kwasababu ya yale yaliyotangulia kufanywa na mikono yao, kisha wakakujia huku wakiapa kwa Allah kwamba: Hatukukusudia ila tu kufanya yaliyo mazuri na kupatanisha?



Sura: ANNISAI 

Aya : 63

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ يَعۡلَمُ ٱللَّهُ مَا فِي قُلُوبِهِمۡ فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ وَعِظۡهُمۡ وَقُل لَّهُمۡ فِيٓ أَنفُسِهِمۡ قَوۡلَۢا بَلِيغٗا

Hao ndio ambao Allah anayajua yaliyomo ndani ya nyoyo zao. Basi wapuuze na wape mawaidha na waambie katika nafsi zao maneno mazito



Sura: ANNISAI 

Aya : 72

وَإِنَّ مِنكُمۡ لَمَن لَّيُبَطِّئَنَّ فَإِنۡ أَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةٞ قَالَ قَدۡ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيَّ إِذۡ لَمۡ أَكُن مَّعَهُمۡ شَهِيدٗا

Na hakika kabisa, wapo miongoni mwenu wanaosuasua (wanaobaki nyuma kwasababu ya kuona uzito wa kutoka kwenda vitani). Ukikupateni msiba wanasema: Hakika, Allah amenineemesha kwa kuwa sikuwa pamoja nao



Sura: ANNISAI 

Aya : 73

وَلَئِنۡ أَصَٰبَكُمۡ فَضۡلٞ مِّنَ ٱللَّهِ لَيَقُولَنَّ كَأَن لَّمۡ تَكُنۢ بَيۡنَكُمۡ وَبَيۡنَهُۥ مَوَدَّةٞ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ مَعَهُمۡ فَأَفُوزَ فَوۡزًا عَظِيمٗا

Na ikikufikieni fadhila itokayo kwa Allah kwa hakika kabisa husema, kama vile hapakuwa na mapenzi yoyote baina yenu na baina yao, kwamba: Laiti nami ningekuwa pamoja nao nikafanikiwa mafanikio makubwa



Sura: ANNISAI 

Aya : 88

۞فَمَا لَكُمۡ فِي ٱلۡمُنَٰفِقِينَ فِئَتَيۡنِ وَٱللَّهُ أَرۡكَسَهُم بِمَا كَسَبُوٓاْۚ أَتُرِيدُونَ أَن تَهۡدُواْ مَنۡ أَضَلَّ ٱللَّهُۖ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَلَن تَجِدَ لَهُۥ سَبِيلٗا

Basi mna nini nyinyi mmegawanyika makundi mawili kuhusu wanafiki, na ilhali Allah amewageuza (na kurudi kwenye ukafiri) kwasababu ya yale waliyo-yachuma? Hivi mnataka kuwaongoa ambao Allah amewapoteza? Na yeyote ambaye Allah amempoteza hutapata njia (ya kumuongoza)



Sura: ANNISAI 

Aya : 89

وَدُّواْ لَوۡ تَكۡفُرُونَ كَمَا كَفَرُواْ فَتَكُونُونَ سَوَآءٗۖ فَلَا تَتَّخِذُواْ مِنۡهُمۡ أَوۡلِيَآءَ حَتَّىٰ يُهَاجِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۚ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَخُذُوهُمۡ وَٱقۡتُلُوهُمۡ حَيۡثُ وَجَدتُّمُوهُمۡۖ وَلَا تَتَّخِذُواْ مِنۡهُمۡ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرًا

Wametamani lau mngekufuru kama walivyokufuru wao ili muwe sawa. Basi msiwafanye marafiki wa karibu miongoni mwao mpaka wahame kwa ajili ya dini ya Allah. Basi kama wakikengeuka washikeni (mateka) na waueni popote mtakapowakuta, na msifanye miongoni mwao rafiki wa karibu wala msaidizi



Sura: ANNISAI 

Aya : 90

إِلَّا ٱلَّذِينَ يَصِلُونَ إِلَىٰ قَوۡمِۭ بَيۡنَكُمۡ وَبَيۡنَهُم مِّيثَٰقٌ أَوۡ جَآءُوكُمۡ حَصِرَتۡ صُدُورُهُمۡ أَن يُقَٰتِلُوكُمۡ أَوۡ يُقَٰتِلُواْ قَوۡمَهُمۡۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَسَلَّطَهُمۡ عَلَيۡكُمۡ فَلَقَٰتَلُوكُمۡۚ فَإِنِ ٱعۡتَزَلُوكُمۡ فَلَمۡ يُقَٰتِلُوكُمۡ وَأَلۡقَوۡاْ إِلَيۡكُمُ ٱلسَّلَمَ فَمَا جَعَلَ ٱللَّهُ لَكُمۡ عَلَيۡهِمۡ سَبِيلٗا

Isipokuwa wale ambao wana-husiana na watu ambao kati yenu na wao kuna mkataba au wamekujieni huku nyoyo zao zikiona tabu kupigana nanyi au kupigana na watu wao. Na Allah angetaka angeliwapa nguvu dhidi yenu wakakupigeni. Basi wakiachana nanyi na wasipigane nanyi na wakakuleteeni amani (wakakutangazieni amani), basi Allah hakukupeni njia (ruhusa ya kupiganana nao)



Sura: ANNISAI 

Aya : 91

سَتَجِدُونَ ءَاخَرِينَ يُرِيدُونَ أَن يَأۡمَنُوكُمۡ وَيَأۡمَنُواْ قَوۡمَهُمۡ كُلَّ مَا رُدُّوٓاْ إِلَى ٱلۡفِتۡنَةِ أُرۡكِسُواْ فِيهَاۚ فَإِن لَّمۡ يَعۡتَزِلُوكُمۡ وَيُلۡقُوٓاْ إِلَيۡكُمُ ٱلسَّلَمَ وَيَكُفُّوٓاْ أَيۡدِيَهُمۡ فَخُذُوهُمۡ وَٱقۡتُلُوهُمۡ حَيۡثُ ثَقِفۡتُمُوهُمۡۚ وَأُوْلَـٰٓئِكُمۡ جَعَلۡنَا لَكُمۡ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٗا مُّبِينٗا

Mtawakuta wengine wanataka kukaa nanyi kwa amani (kwa kuonesha kuwa nao wameamini) na kukaa kwa amani na watu wao (kwa kuwaonesha kuwa bado wao ni makafiri). Kila wanaporudishwa kwenye fitina (ukafiri) wanaporomoshwa (wanaburuzwa na kurudi kwa kasi kubwa) kwenye ukafiri huo. Basi kama hawakukuacheni na hawakukutangazieni amani na hawakuizuia mikono yao (wakaacha kukupigeni), basi wakamateni na waueni popote mtakapowakuta, na hao tumekupeni hoja ya wazi (ya kuwashambulia, kuwapiga, kuwaua na kuwakamata mateka)



Sura: ANNISAI 

Aya : 138

بَشِّرِ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ بِأَنَّ لَهُمۡ عَذَابًا أَلِيمًا

Wape bishara[1] wanafiki kwamba wanayo adhabu iumizayo mno


1- - Bishara ni taarifa ya jambo jema linaloleta faraja. Adhabu sio jambo jema la kutia faraja, lakini hapa limetumika kwa wanafiki kwa madhumuni ya kuwakejeli na kuwadhihaki.


Sura: ANNISAI 

Aya : 139

ٱلَّذِينَ يَتَّخِذُونَ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۚ أَيَبۡتَغُونَ عِندَهُمُ ٱلۡعِزَّةَ فَإِنَّ ٱلۡعِزَّةَ لِلَّهِ جَمِيعٗا

(Wanafiki) Ambao wanawafanya makafiri kuwa marafiki badala ya Waumini (wenzao). Hivi wanatafuta heshima kwao? Basi hakika, heshima yote ni miliki ya Allah tu



Sura: ANNISAI 

Aya : 140

وَقَدۡ نَزَّلَ عَلَيۡكُمۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ أَنۡ إِذَا سَمِعۡتُمۡ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ يُكۡفَرُ بِهَا وَيُسۡتَهۡزَأُ بِهَا فَلَا تَقۡعُدُواْ مَعَهُمۡ حَتَّىٰ يَخُوضُواْ فِي حَدِيثٍ غَيۡرِهِۦٓ إِنَّكُمۡ إِذٗا مِّثۡلُهُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ جَامِعُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡكَٰفِرِينَ فِي جَهَنَّمَ جَمِيعًا

Na kwa hakika, (Allah) amekuteremshieni katika kitabu (Qur’ani) kwamba msikiapo Aya za Allah zinakanushwa na zinafanyiwa kejeli, basi msikae pamoja nao (hao wafanyao hivyo), mpaka waingie katika mazungumzo mengine[1]. Hakika, mkikaa nao nanyi mtakuwa kama wao. Hakika, Allah atawakusanya Wanafiki na Makafiri wote katika Jahanamu


1- - Allah ametaja suala hili katika Aya ya 68 ya Sura Al-an-aam (6) inayosema kwamba “Na ukiwaona wanaozisema vibaya Aya zetu usikae nao…”.


Sura: ANNISAI 

Aya : 141

ٱلَّذِينَ يَتَرَبَّصُونَ بِكُمۡ فَإِن كَانَ لَكُمۡ فَتۡحٞ مِّنَ ٱللَّهِ قَالُوٓاْ أَلَمۡ نَكُن مَّعَكُمۡ وَإِن كَانَ لِلۡكَٰفِرِينَ نَصِيبٞ قَالُوٓاْ أَلَمۡ نَسۡتَحۡوِذۡ عَلَيۡكُمۡ وَنَمۡنَعۡكُم مِّنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۚ فَٱللَّهُ يَحۡكُمُ بَيۡنَكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ وَلَن يَجۡعَلَ ٱللَّهُ لِلۡكَٰفِرِينَ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ سَبِيلًا

Ambao wanakuvizieni. Mkipata ushindi unaotoka kwa Allah wanasema: Si tulikuwa pamoja na nyinyi? Na ikiwa makafiri wamepata sehemu ndogo ya ushindi wanasema: Si tulikusimamieni na kukukingeni dhidi ya Waislamu? Basi Allah atahukumu baina yenu Siku ya Kiama. Na Allah hatawapa makafiri njia (ya kuwashinda) Waislamu



Sura: ANNISAI 

Aya : 142

إِنَّ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ يُخَٰدِعُونَ ٱللَّهَ وَهُوَ خَٰدِعُهُمۡ وَإِذَا قَامُوٓاْ إِلَى ٱلصَّلَوٰةِ قَامُواْ كُسَالَىٰ يُرَآءُونَ ٱلنَّاسَ وَلَا يَذۡكُرُونَ ٱللَّهَ إِلَّا قَلِيلٗا

Hakika, wanafiki wanamhadaa Allah, naye ni mwenye kuwahadaa (pia). Na wanaposimama kwenda kuswali wanasimama wakiwa wavivu, wanajionyesha kwa watu (kwamba nao ni Waislamu) na hawamtaji Allah isipokuwa kidogo sana



Sura: ANNISAI 

Aya : 143

مُّذَبۡذَبِينَ بَيۡنَ ذَٰلِكَ لَآ إِلَىٰ هَـٰٓؤُلَآءِ وَلَآ إِلَىٰ هَـٰٓؤُلَآءِۚ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَلَن تَجِدَ لَهُۥ سَبِيلٗا

Wanayumba yumba baina ya hayo (ya hali mbili za imani na unafiki). Hawako kwa hawa (Waislamu) na hawako kwa hawa (makafiri). Na yeyote ambaye Allah amempoteza hutampatia njia yoyote (ya kumuongoa)