Sura: AL-AN’AAM 

Aya : 84

وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَۚ كُلًّا هَدَيۡنَاۚ وَنُوحًا هَدَيۡنَا مِن قَبۡلُۖ وَمِن ذُرِّيَّتِهِۦ دَاوُۥدَ وَسُلَيۡمَٰنَ وَأَيُّوبَ وَيُوسُفَ وَمُوسَىٰ وَهَٰرُونَۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na tulimtunuku (Mtume Ibrahimu) Isihaka na Yakubu. Wote tuliwaongoa. Na Nuhu tulimuongoa kabla (yao). Na katika kizazi chake tulimongoa Daudi na Suleimani na Ayubu na Yusufu na Mussa na Haruna. Na kama hivyo tunawalipa wafanyao mazuri



Sura: HUUD 

Aya : 71

وَٱمۡرَأَتُهُۥ قَآئِمَةٞ فَضَحِكَتۡ فَبَشَّرۡنَٰهَا بِإِسۡحَٰقَ وَمِن وَرَآءِ إِسۡحَٰقَ يَعۡقُوبَ

Na mkewe alikuwa kasimama, na akacheka. Basi tukambashiria (kuzaliwa mtoto) Is-haq, na baada ya Is-haq Yakubu



Sura: IBRAHIM 

Aya : 39

ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي وَهَبَ لِي عَلَى ٱلۡكِبَرِ إِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَۚ إِنَّ رَبِّي لَسَمِيعُ ٱلدُّعَآءِ

Himdi zote ni za Allah aliyenitunuku (watoto) katika hali ya uzee, Ismail na Is-haq. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kusikia maombi



Sura: MARYAM 

Aya : 49

فَلَمَّا ٱعۡتَزَلَهُمۡ وَمَا يَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَۖ وَكُلّٗا جَعَلۡنَا نَبِيّٗا

Basi alipo jitenga nao na yale waliyo kuwa wakiyaabudu badala ya Allah, tulimpa Is-haq na Yaaqub, na kila mmoja tukamfanya Nabii



Sura: AL-ANBIYAA 

Aya : 72

وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ نَافِلَةٗۖ وَكُلّٗا جَعَلۡنَا صَٰلِحِينَ

Naye tukampa Is-haq, na Yaaqub kuwa ni ziada. Na wote tukawajaalia wawe watu wema



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 112

وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 113

وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٞ وَظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٞ

Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa vizazi vyao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi



Sura: SWAAD 

Aya : 45

وَٱذۡكُرۡ عِبَٰدَنَآ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ أُوْلِي ٱلۡأَيۡدِي وَٱلۡأَبۡصَٰرِ

Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa’qubu waliokuwa na nguvu na busara