Sura: AL-IMRAN 

Aya : 91

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَمَاتُواْ وَهُمۡ كُفَّارٞ فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡ أَحَدِهِم مِّلۡءُ ٱلۡأَرۡضِ ذَهَبٗا وَلَوِ ٱفۡتَدَىٰ بِهِۦٓۗ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ وَمَا لَهُم مِّن نَّـٰصِرِينَ

Hakika, wale waliokufuru na wakafa wakiwa makafiri, kamwe hatakubaliwa mmoja wao hata kama atajikomboa kwa kutoa fidia ya dhahabu ujazo wa ardhi yote. Hao watapata adhabu yenye maumivu makali mno na hawatakuwa na watetezi (wowote)



Sura: AL-MAIDA 

Aya : 36

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡ أَنَّ لَهُم مَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا وَمِثۡلَهُۥ مَعَهُۥ لِيَفۡتَدُواْ بِهِۦ مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ مَا تُقُبِّلَ مِنۡهُمۡۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Hakika ya wale waliokufuru, lau kama wangekuwa na yote yaliyomo duniani na mengine kama hayo ili watoe fidia ya kuepukana na adhabu ya Siku ya Kiyama, wasingekubaliwa, na watapata adhabu iumizayo



Sura: YUNUS 

Aya : 54

وَلَوۡ أَنَّ لِكُلِّ نَفۡسٖ ظَلَمَتۡ مَا فِي ٱلۡأَرۡضِ لَٱفۡتَدَتۡ بِهِۦۗ وَأَسَرُّواْ ٱلنَّدَامَةَ لَمَّا رَأَوُاْ ٱلۡعَذَابَۖ وَقُضِيَ بَيۡنَهُم بِٱلۡقِسۡطِ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na lau kama kila nafsi iliyodhu-lumu ingekuwa inamiliki vyote vilivyomo duniani, bila shaka yoyote ingevitoa fidia (ili kujikomboa isiadhibiwe). Na watakapoiona adhabu wataficha majuto na patahu-kumiwa baina yao kwa uadilifu, nao hawatadhulumiwa



Sura: AR-RA’D 

Aya : 18

لِلَّذِينَ ٱسۡتَجَابُواْ لِرَبِّهِمُ ٱلۡحُسۡنَىٰۚ وَٱلَّذِينَ لَمۡ يَسۡتَجِيبُواْ لَهُۥ لَوۡ أَنَّ لَهُم مَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا وَمِثۡلَهُۥ مَعَهُۥ لَٱفۡتَدَوۡاْ بِهِۦٓۚ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ سُوٓءُ ٱلۡحِسَابِ وَمَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ

Wale waliomuitikia Mola wao Mlezi watapata wema (Pepo). Na wale wasiomuitikia, hata wangelikuwa na vyote vilivyomo katika ardhi na mfano wa hivyo, bila ya shaka wangevitoa kujikomboa. Hao watakuwa na hesabu mbaya, na makao yao ni Jahanamu. Napo ni mahala pabaya mno



Sura: AZZUMAR 

Aya : 47

وَلَوۡ أَنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ مَا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا وَمِثۡلَهُۥ مَعَهُۥ لَٱفۡتَدَوۡاْ بِهِۦ مِن سُوٓءِ ٱلۡعَذَابِ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ وَبَدَا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مَا لَمۡ يَكُونُواْ يَحۡتَسِبُونَ

Na lau kuwa walio dhulumu wangeli kuwa na vyote viliomo duniani na pamoja navyo vingine kama hivyo, bila ya shaka wangeli vitoa kujikomboa katika adhabu mbaya Siku hiyo ya Kiyama. Na yatawadhihirikia kwa Allah wasiyo kuwa wakiyatarajia



Sura: AL-HADIID

Aya : 15

فَٱلۡيَوۡمَ لَا يُؤۡخَذُ مِنكُمۡ فِدۡيَةٞ وَلَا مِنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ مَأۡوَىٰكُمُ ٱلنَّارُۖ هِيَ مَوۡلَىٰكُمۡۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Basi leo haitochukuliwa kutoka kwenu fidia na wala kutoka kwa waliokufuru. Makazi yenu ni moto, hayo ndio yanayostahiki kwenu, na ni marejeo mabaya yalioje



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 11

يُبَصَّرُونَهُمۡۚ يَوَدُّ ٱلۡمُجۡرِمُ لَوۡ يَفۡتَدِي مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِئِذِۭ بِبَنِيهِ

Watafanywa waonane. Mkosefu atatamani (kujikomboa) ajitolee fidia kutokana na adhabu Siku hiyo kwa kuwatoa watoto wake