Sura: AL-INSAAN

Aya : 22

إِنَّ هَٰذَا كَانَ لَكُمۡ جَزَآءٗ وَكَانَ سَعۡيُكُم مَّشۡكُورًا

(Wataambiwa) Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 25

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ

Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika



Sura: AL-FAJRI 

Aya : 27

يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!



Sura: AL-FAJRI 

Aya : 28

ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha



Sura: AL-FAJRI 

Aya : 29

فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,



Sura: AL-FAJRI 

Aya : 30

وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي

Na ingia katika Pepo yangu



Sura: ATTIIN 

Aya : 6

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ

Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 7

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمۡ خَيۡرُ ٱلۡبَرِيَّةِ

Hakika walio amini na wakatenda mema, hao ndio bora wa viumbe



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 8

جَزَآؤُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتُ عَدۡنٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ ذَٰلِكَ لِمَنۡ خَشِيَ رَبَّهُۥ

Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za daima, zipitazo mito kati yake. Wakae humo milele. Allah yupo radhi nao, na wao waporadhi naye. Hayo ni kwa anaye muogopa Mola wake Mlezi