Sura: SWAAD 

Aya : 80

قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ

Allah akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,



Sura: SWAAD 

Aya : 81

إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ

Mpaka siku ya wakati maalumu



Sura: SWAAD 

Aya : 82

قَالَ فَبِعِزَّتِكَ لَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,



Sura: SWAAD 

Aya : 83

إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio chaguliwa



Sura: SWAAD 

Aya : 84

قَالَ فَٱلۡحَقُّ وَٱلۡحَقَّ أَقُولُ

Akasema: Haki! Na haki ninaisema



Sura: SWAAD 

Aya : 85

لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكَ وَمِمَّن تَبِعَكَ مِنۡهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao



Sura: AZZUKHRUF 

Aya : 62

وَلَا يَصُدَّنَّكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُۖ إِنَّهُۥ لَكُمۡ عَدُوّٞ مُّبِينٞ

Wala asikuzuilieni Shetani. Hakika yeye ni adui yenu wa dhaahiri



Sura: MUHAMMAD 

Aya : 25

إِنَّ ٱلَّذِينَ ٱرۡتَدُّواْ عَلَىٰٓ أَدۡبَٰرِهِم مِّنۢ بَعۡدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمُ ٱلۡهُدَى ٱلشَّيۡطَٰنُ سَوَّلَ لَهُمۡ وَأَمۡلَىٰ لَهُمۡ

Kwa hakika wanao rudi nyuma baada ya kuwabainikia uongofu, Shetani amewashawishi na amewadanganya



Sura: AL-MUJAADILA 

Aya : 10

إِنَّمَا ٱلنَّجۡوَىٰ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ لِيَحۡزُنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَيۡسَ بِضَآرِّهِمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ

Hakika mnong’ono unatokana na shaytwaan ili awahuzunishe wale walioamini, na wala hawezi kuwadhuru chochote isipokuwa kwa idhini ya Allah. Na kwa Allah wategemee wenye kuaumini



Sura: AL-MUJAADILA 

Aya : 19

ٱسۡتَحۡوَذَ عَلَيۡهِمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ فَأَنسَىٰهُمۡ ذِكۡرَ ٱللَّهِۚ أُوْلَـٰٓئِكَ حِزۡبُ ٱلشَّيۡطَٰنِۚ أَلَآ إِنَّ حِزۡبَ ٱلشَّيۡطَٰنِ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Shetani amewatawala, akawasahaulisha kumkumbuka Allah, hao ndio kundi la shetani. Zindukeni! Hakika kundi la shetani ndio lenye kukhasirika. (lenye kupata khasara)



Sura: AL-HASHRI 

Aya : 16

كَمَثَلِ ٱلشَّيۡطَٰنِ إِذۡ قَالَ لِلۡإِنسَٰنِ ٱكۡفُرۡ فَلَمَّا كَفَرَ قَالَ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّنكَ إِنِّيٓ أَخَافُ ٱللَّهَ رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

(Wanafiki) Ni kama mfano wa Shetani anapo mwambia mtu: Kufuru. Na akikufuru humwambia: Mimi si pamoja nawe. Hakika mimi namwogopa Allah, Mola wa walimwengu wote