Sura: ASH-SHUURAA 

Aya : 5

تَكَادُ ٱلسَّمَٰوَٰتُ يَتَفَطَّرۡنَ مِن فَوۡقِهِنَّۚ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يُسَبِّحُونَ بِحَمۡدِ رَبِّهِمۡ وَيَسۡتَغۡفِرُونَ لِمَن فِي ٱلۡأَرۡضِۗ أَلَآ إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ

Mbingu zinakaribia kuwa-pasukia, na Malaika wanamtakasa Mola wao Mlezi kwa kumhimidi, na wanawaombea msamaha (waumini) waliomo kwenye ardhi. Zindukeni! Hakika, Allah ni Mwenye kusamehe sana, Mwenye kurehemu



Sura: AZZUKHRUF 

Aya : 77

وَنَادَوۡاْ يَٰمَٰلِكُ لِيَقۡضِ عَلَيۡنَا رَبُّكَۖ قَالَ إِنَّكُم مَّـٰكِثُونَ

Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi! Naye aseme: Hakika nyinyi mtakaa humo humo!



Sura: AZZUKHRUF 

Aya : 80

أَمۡ يَحۡسَبُونَ أَنَّا لَا نَسۡمَعُ سِرَّهُمۡ وَنَجۡوَىٰهُمۚ بَلَىٰ وَرُسُلُنَا لَدَيۡهِمۡ يَكۡتُبُونَ

Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong’ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika



Sura: QAAF 

Aya : 17

إِذۡ يَتَلَقَّى ٱلۡمُتَلَقِّيَانِ عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ قَعِيدٞ

Pale wanapopokea wapokeaji wawili (Malaika) wanaokaa kuliani na kushotoni



Sura: QAAF 

Aya : 18

مَّا يَلۡفِظُ مِن قَوۡلٍ إِلَّا لَدَيۡهِ رَقِيبٌ عَتِيدٞ

Hatamki kauli yoyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi)



Sura: QAAF 

Aya : 21

وَجَآءَتۡ كُلُّ نَفۡسٖ مَّعَهَا سَآئِقٞ وَشَهِيدٞ

Na kila nafsi itakuja pamoja nayo mcungaji na shahidi



Sura: QAAF 

Aya : 22

لَّقَدۡ كُنتَ فِي غَفۡلَةٖ مِّنۡ هَٰذَا فَكَشَفۡنَا عَنكَ غِطَآءَكَ فَبَصَرُكَ ٱلۡيَوۡمَ حَدِيدٞ

(Aambiwe): Kwa yakini ulikuwa umeghafilika na haya! Basi Tumekuondoshea kifuniko chako (pazia lako), basi kuona kwako leo ni kukali



Sura: QAAF 

Aya : 23

وَقَالَ قَرِينُهُۥ هَٰذَا مَا لَدَيَّ عَتِيدٌ

Na Malaika wake aliyepewa jukumu atasema: Hii (rekodi) iliyoko kwangu imeshatayarishwa



Sura: ANNAJMI 

Aya : 26

۞وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ

Na kuna malaika wengi mbinguni hainufaishi chochote uombezi wao ila baada ya kupewa idhini na Allah kwa amtakaye na amridhie



Sura: ANNAJMI 

Aya : 27

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ

Hakika wale wasioamini Aakhirah bila shaka wanawaita Malaika kwa majina ya kike



Sura: ANNAJMI 

Aya : 28

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا

Na wala hawana ujuzi wowote ule wa hayo; hawafuati isipokuwa dhana, na hakika dhana haifai kitu chochote mbele ya haki



Sura: ATTAHRIIM 

Aya : 6

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ وَأَهۡلِيكُمۡ نَارٗا وَقُودُهَا ٱلنَّاسُ وَٱلۡحِجَارَةُ عَلَيۡهَا مَلَـٰٓئِكَةٌ غِلَاظٞ شِدَادٞ لَّا يَعۡصُونَ ٱللَّهَ مَآ أَمَرَهُمۡ وَيَفۡعَلُونَ مَا يُؤۡمَرُونَ

Enyi walioamini! Jikingeni nafsi zenu na ahli zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe; Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu, hawamuasi Allah kwa yale Anayowaamrisha na wanafanya yale wanayoamrishwa



Sura: ALHAAQQA 

Aya : 17

وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ

Na Malaika Watakuwa Wame-simama Kandoni Mwake, Na Siku Hiyo Juu Yao Malaika Wanane Watakibeba Kiti Cha Enzi Cha Mola Wako



Sura: ALMA’RIJ 

Aya : 4

تَعۡرُجُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيۡهِ فِي يَوۡمٖ كَانَ مِقۡدَارُهُۥ خَمۡسِينَ أَلۡفَ سَنَةٖ

Malaika na Roho (Jibrili) wanapanda kwenda kwake katika siku ambayo makadirio yake ni miaka hamsini elfu



Sura: ALJINN 

Aya : 27

إِلَّا مَنِ ٱرۡتَضَىٰ مِن رَّسُولٖ فَإِنَّهُۥ يَسۡلُكُ مِنۢ بَيۡنِ يَدَيۡهِ وَمِنۡ خَلۡفِهِۦ رَصَدٗا

Isipo kuwa Mtume wake aliye mridhia. Naye huyo humwekea walinzi mbele yake na nyuma yake



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 31

وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَـٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ

Na Hatukuweka walinzi wa moto isipokuwa ni Malaika, na Hatukufanya idadi yao isipokuwa iwe ni mtihani kwa wale waliokufuru; ili wawe na yakini wale waliopewa Kitabu, na iwazidishie Imani wale walioamini; na wala wasitie shaka wale waliopewa Kitabu na Waumini; na ili wale waliokuwa na maradhi nyoyoni mwao (ya unafiki), na makafiri waseme: Allah Amekusudia nini kwa mfano huu? Hivyo ndivyo Allah Anavyompoteza Amtakaye na Anamuongoa Amtakaye. Na hakuna ajuaye majeshi ya Mola wako isipokuwa Yeye Peke yake, na haya hayakuwa isipokuwa ni ukumbusho tu kwa binadamu



Sura: ANNABAI 

Aya : 38

يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا

Siku atakayosimama Roho (Jibrili) na Malaika hali ya kujipanga safu; Hawatasema ila aliye mruhusu Mwingi wa rehema, na atasema yaliyo sawa tu



Sura: ANNAAZIAAT 

Aya : 1

وَٱلنَّـٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا

Nina apa kwa [Malaika] wanaong’oa (roho) kwa nguvu



Sura: ANNAAZIAAT 

Aya : 2

وَٱلنَّـٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا

Na (kwa Malaika) wanaotoa (roho) kwa upole



Sura: ANNAAZIAAT 

Aya : 3

وَٱلسَّـٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا

Na ( kwa Malaika) wanaoogelea sana (katika anga kwa kupanda na kushuka wakitekeleza majukumu waliyopewa na Allah)



Sura: ANNAAZIAAT 

Aya : 4

فَٱلسَّـٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا

Kisha (Nina apa kwa Malaika) wenye kuongoza (katika kushidana wakati wa kutimiza wajibu wao)



Sura: ANNAAZIAAT 

Aya : 5

فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا

Kisha (Nina apa kwa Malaika) wenye kuendesha kila jambo (kwa maagizo ya Allah)



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 10

وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ

Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 11

كِرَامٗا كَٰتِبِينَ

Waandishi wenye hishima,



Sura: AL-INFITWAAR 

Aya : 12

يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ

Wanayajua mnayo yatenda



Sura: AL-FAJRI 

Aya : 22

وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 18

سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ

Nasi tutawaita Mazabania!



Sura: AL-QADRI 

Aya : 4

تَنَزَّلُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ فِيهَا بِإِذۡنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمۡرٖ

Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo