Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 196

وَأَتِمُّواْ ٱلۡحَجَّ وَٱلۡعُمۡرَةَ لِلَّهِۚ فَإِنۡ أُحۡصِرۡتُمۡ فَمَا ٱسۡتَيۡسَرَ مِنَ ٱلۡهَدۡيِۖ وَلَا تَحۡلِقُواْ رُءُوسَكُمۡ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ ٱلۡهَدۡيُ مَحِلَّهُۥۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوۡ بِهِۦٓ أَذٗى مِّن رَّأۡسِهِۦ فَفِدۡيَةٞ مِّن صِيَامٍ أَوۡ صَدَقَةٍ أَوۡ نُسُكٖۚ فَإِذَآ أَمِنتُمۡ فَمَن تَمَتَّعَ بِٱلۡعُمۡرَةِ إِلَى ٱلۡحَجِّ فَمَا ٱسۡتَيۡسَرَ مِنَ ٱلۡهَدۡيِۚ فَمَن لَّمۡ يَجِدۡ فَصِيَامُ ثَلَٰثَةِ أَيَّامٖ فِي ٱلۡحَجِّ وَسَبۡعَةٍ إِذَا رَجَعۡتُمۡۗ تِلۡكَ عَشَرَةٞ كَامِلَةٞۗ ذَٰلِكَ لِمَن لَّمۡ يَكُنۡ أَهۡلُهُۥ حَاضِرِي ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Na timizeni Hija na Umra kwa ajili ya Allah. Na ikiwa mmezuiwa[1], basi chinjeni wanyama watakaokuwa rahisi kupatikana. Na wala msinyoe vichwa vyenu, hadi mnyama afike mahali pake. Basi ambaye atakuwa mgonjwa miongoni mwenu, au ana tatizo kichwani kwake, basi atoe fidia ya kufunga au sadaka au mnyama. Na mtakapokuwa katika hali ya amani, atakayefanya Umra kabla ya Hija[2] basi afunge siku tatu katika Hija na siku saba mtakaporejea kwenu. Hizo ni siku kumi kamili. Hilo ni kwa ambaye familia yake sio wakazi wa (mji wa) Msikiti Mtukufu (wa Makka). Na mcheni Allah, na jueni kwamba, Allah ni mkali wa kuadhibu


1- - Kutimiza ibada hizo


2- - Bila kuunganisha Umra na Hija


Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 215

يَسۡـَٔلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَۖ قُلۡ مَآ أَنفَقۡتُم مِّنۡ خَيۡرٖ فَلِلۡوَٰلِدَيۡنِ وَٱلۡأَقۡرَبِينَ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِۗ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٞ

Wanakuuliza: Watoe nini? Sema: Chochote cha heri mtakachotoa basi wapeni wazazi na ndugu na Mayatima na masikini na Msafiri na heri yoyote muifanyayo kwa hakika Allah anaijua mno



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 254

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَنفِقُواْ مِمَّا رَزَقۡنَٰكُم مِّن قَبۡلِ أَن يَأۡتِيَ يَوۡمٞ لَّا بَيۡعٞ فِيهِ وَلَا خُلَّةٞ وَلَا شَفَٰعَةٞۗ وَٱلۡكَٰفِرُونَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Enyi mlioamini, toeni katika vile tulivyowapeni kabla haijafika siku ambayo haitakuwa na mauzo wala urafiki wala uombezi, na makafiri ndio wenye kudhulumu



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 261

مَّثَلُ ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ كَمَثَلِ حَبَّةٍ أَنۢبَتَتۡ سَبۡعَ سَنَابِلَ فِي كُلِّ سُنۢبُلَةٖ مِّاْئَةُ حَبَّةٖۗ وَٱللَّهُ يُضَٰعِفُ لِمَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٌ

Mfano wa wale wanaotoa mali zao katika njia ya Allah ni kama mfano wa punje iliyotoa mashuke saba, ikawa katika kila shuke mna punje mia. Na Allah humuongezea amtakaye, Na Allah ni Mwingi wa fadhila, Mjuzi mno



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 262

ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ ثُمَّ لَا يُتۡبِعُونَ مَآ أَنفَقُواْ مَنّٗا وَلَآ أَذٗى لَّهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Wale wanaotoa mali zao katika njia ya Allah, kisha wasifuatishe yale waliyoyatoa kwa masimbulizi wala maudhi, wana malipo yao kwa Mola wao, wala hawatakuwa na hofu na hawatahuzunika



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 263

۞قَوۡلٞ مَّعۡرُوفٞ وَمَغۡفِرَةٌ خَيۡرٞ مِّن صَدَقَةٖ يَتۡبَعُهَآ أَذٗىۗ وَٱللَّهُ غَنِيٌّ حَلِيمٞ

Kauli njema na kusamehe ni bora kuliko sadaka inayofuatishwa na maudhi, na Allah ni Mkwasi sana, Mpole mno



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 264

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُبۡطِلُواْ صَدَقَٰتِكُم بِٱلۡمَنِّ وَٱلۡأَذَىٰ كَٱلَّذِي يُنفِقُ مَالَهُۥ رِئَآءَ ٱلنَّاسِ وَلَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۖ فَمَثَلُهُۥ كَمَثَلِ صَفۡوَانٍ عَلَيۡهِ تُرَابٞ فَأَصَابَهُۥ وَابِلٞ فَتَرَكَهُۥ صَلۡدٗاۖ لَّا يَقۡدِرُونَ عَلَىٰ شَيۡءٖ مِّمَّا كَسَبُواْۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Enyi mlioamini, msizibatilishe sadaka zenu kwa masimbulizi na maudhi, kama yule anayetoa mali yake kwa kuwaonesha watu, na hamuamini Allah na Siku ya Mwisho. Basi mfano wake ni kama jiwe lenye kuteleza ambalo juu yake kuna mchanga, kisha likanyeshewa na mvua kubwa na ikaliacha tupu. Basi hawatakuwa na uwezo juu ya chochote katika walicho kichuma, na Allah hawaongozi watu makafiri



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 265

وَمَثَلُ ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمُ ٱبۡتِغَآءَ مَرۡضَاتِ ٱللَّهِ وَتَثۡبِيتٗا مِّنۡ أَنفُسِهِمۡ كَمَثَلِ جَنَّةِۭ بِرَبۡوَةٍ أَصَابَهَا وَابِلٞ فَـَٔاتَتۡ أُكُلَهَا ضِعۡفَيۡنِ فَإِن لَّمۡ يُصِبۡهَا وَابِلٞ فَطَلّٞۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٌ

Na mfano wa wale wanaotoa mali zao kwa kuzitafuta radhi za Allah kwa uthabiti na yakini wa nafsi zao, ni kama mfano wa bustani iliyo katika muinuko, ipatayo mvua nyingi, na ikatoa matunda yake maradufu, na isiponyeshewa na mvua nyingi, mvua chache (hutosha) na Allah anayajua mnayoyatenda



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 267

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَنفِقُواْ مِن طَيِّبَٰتِ مَا كَسَبۡتُمۡ وَمِمَّآ أَخۡرَجۡنَا لَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِۖ وَلَا تَيَمَّمُواْ ٱلۡخَبِيثَ مِنۡهُ تُنفِقُونَ وَلَسۡتُم بِـَٔاخِذِيهِ إِلَّآ أَن تُغۡمِضُواْ فِيهِۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ غَنِيٌّ حَمِيدٌ

Enyi mlioamini, toeni katika vitu vizuri mlivyovichuma, na katika vile tulivyowatoleeni kutoka katika ardhi. Na msikusudie (kutoa) kibaya na hali nyinyi hamkuwa ni wenye kukipokea (kama mtapewa) ila kwa kukifumbia macho, najueni kwamba, Allah ni Mkwasi, Mwenye kuhimidiwa mno



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 270

وَمَآ أَنفَقۡتُم مِّن نَّفَقَةٍ أَوۡ نَذَرۡتُم مِّن نَّذۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُهُۥۗ وَمَا لِلظَّـٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٍ

Na chochote mkitoacho au nadhiri yoyote muiwekayo kwa hakika Allah anaijua, na madhalimu hawana yeyote wa kuwanusuru



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 271

إِن تُبۡدُواْ ٱلصَّدَقَٰتِ فَنِعِمَّا هِيَۖ وَإِن تُخۡفُوهَا وَتُؤۡتُوهَا ٱلۡفُقَرَآءَ فَهُوَ خَيۡرٞ لَّكُمۡۚ وَيُكَفِّرُ عَنكُم مِّن سَيِّـَٔاتِكُمۡۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Iwapo mtadhihirisha sadaka ni vizuri sana, na kama mtatoa kwa siri na kuwapa mafukara basi hilo ni bora zaidi kwenu na atakufutieni baadhi ya maovu yenu na Allah anayajua mno mnayoyatenda



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 272

۞لَّيۡسَ عَلَيۡكَ هُدَىٰهُمۡ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يَهۡدِي مَن يَشَآءُۗ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَلِأَنفُسِكُمۡۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ ٱللَّهِۚ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ يُوَفَّ إِلَيۡكُمۡ وَأَنتُمۡ لَا تُظۡلَمُونَ

Si jukumu lako kuwaongoa, lakini Allah humuongoa amtakaye. Na heri yoyote muitoayo, basi ni kwa (manufaa ya) nafsi zenu. Na msitoe ila kwa kutafuta wajihi (radhi) za Allah, na heri yoyote mtakayotoa mtarudishiwa kamili, nanyi hamtadhulumiwa



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 273

لِلۡفُقَرَآءِ ٱلَّذِينَ أُحۡصِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا يَسۡتَطِيعُونَ ضَرۡبٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ يَحۡسَبُهُمُ ٱلۡجَاهِلُ أَغۡنِيَآءَ مِنَ ٱلتَّعَفُّفِ تَعۡرِفُهُم بِسِيمَٰهُمۡ لَا يَسۡـَٔلُونَ ٱلنَّاسَ إِلۡحَافٗاۗ وَمَا تُنفِقُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٌ

(Heri na sadaka hizo) Wapewe mafakiri waliofungwa katika njia ya Allah wasioweza kusafiri katika ardhi (kwa kujitafutia riziki), asiyewajua huwadhania ni wakwasi kwa kujizuia kuomba. Utawatambua kwa alama zao, hawawaombi watu kwa ung’ang’anizi. Na heri yoyote mnayoitoa, basi kwa hakika Allah anaijua sana



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 274

ٱلَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُم بِٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِ سِرّٗا وَعَلَانِيَةٗ فَلَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Wale watoao mali zao usiku na mchana, kwa siri na kwa dhahiri, basi wana malipo yao kwa Mola wao, na hawatakuwa na hofu yoyote na hawatahuzunika



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 276

يَمۡحَقُ ٱللَّهُ ٱلرِّبَوٰاْ وَيُرۡبِي ٱلصَّدَقَٰتِۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ كَفَّارٍ أَثِيمٍ

Allah huiondolea baraka riba na huzibariki sadaka, na Allah hampendi kila kafiri mno mwingi wa dhambi



Sura: AL-BAQARAH 

Aya : 280

وَإِن كَانَ ذُو عُسۡرَةٖ فَنَظِرَةٌ إِلَىٰ مَيۡسَرَةٖۚ وَأَن تَصَدَّقُواْ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na kama (mdeni) ni mwenye hali ngumu, basi (mdai) angoje mpaka wakati wa uwezo. Na kulifanya sadaka (hilo deni) ni heri kwenu (kuliko kungoja mpaka mdaiwa kupata uwezo), ikiwa mnajua



Sura: AL-IMRAN 

Aya : 92

لَن تَنَالُواْ ٱلۡبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُواْ مِمَّا تُحِبُّونَۚ وَمَا تُنفِقُواْ مِن شَيۡءٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٞ

Hamtaupata wema hadi mtoe katika mnavyovipenda. Na kitu chochote mtakachokitoa, hakika Allah anakijua sana



Sura: ANNISAI 

Aya : 92

وَمَا كَانَ لِمُؤۡمِنٍ أَن يَقۡتُلَ مُؤۡمِنًا إِلَّا خَطَـٔٗاۚ وَمَن قَتَلَ مُؤۡمِنًا خَطَـٔٗا فَتَحۡرِيرُ رَقَبَةٖ مُّؤۡمِنَةٖ وَدِيَةٞ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦٓ إِلَّآ أَن يَصَّدَّقُواْۚ فَإِن كَانَ مِن قَوۡمٍ عَدُوّٖ لَّكُمۡ وَهُوَ مُؤۡمِنٞ فَتَحۡرِيرُ رَقَبَةٖ مُّؤۡمِنَةٖۖ وَإِن كَانَ مِن قَوۡمِۭ بَيۡنَكُمۡ وَبَيۡنَهُم مِّيثَٰقٞ فَدِيَةٞ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ وَتَحۡرِيرُ رَقَبَةٖ مُّؤۡمِنَةٖۖ فَمَن لَّمۡ يَجِدۡ فَصِيَامُ شَهۡرَيۡنِ مُتَتَابِعَيۡنِ تَوۡبَةٗ مِّنَ ٱللَّهِۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمٗا

Na haiwi kwa Muumini (Muis-lamu) yeyote kumuua Muumini (mwingine) isipokuwa tu kwa kukosea. Na yeyote aliyemuua Muumini kwa kukosea, basi (adhabu yake) ni kuacha huru mtumwa Muumini (Muislamu) na Dia (fidia)[1] itakayokabidhiwa kwa ndugu zake (warithi wake), isipokuwa tu kama (ndugu hao) watafanya Dia hiyo sadaka (kwa kusamehe). Na kama (aliyeuliwa) ni kutoka kwa watu maadui wenu (makafiri), na yeye (marehemu) ni Mumini (Muislamu), basi (adhabu ya muuaji) ni kuacha huru mtumwa Muislamu tu.[2] Na kama (aliyeuliwa) ni kutoka kwa watu (makafiri) ambao kuna mkataba kati yenu na wao (wa kuishi kwa amani) basi (adhabu ya muuaji) ni Dia (fidia) itakayokabidhiwa kwa ndugu zake na kuacha huru mtumwa Muislamu[3]. Basi ambaye hakupata (mtumwa wa kumuacha huru adhabu yake) ni kufunga miezi miwili mfululizo. (Hii) Ndio toba kutoka kwa Allah, na Allah ni Mjuzi sana, Mwenye hekima nyingi


1- - Dia au fidia ya kuua ni ngamia mia moja (100) kama alivyoainisha Mtume, Allah amshushie rehema na amani, katika waraka alioutuma kwa watu wa Yemen. Ameyanukuu haya Imamu Malik katika kitabu chake cha Muwattwai.


2- - Hapa aya inamaanisha kuwa aliyeuliwa ni Muislamu lakini ndugu zake ni makafiri. Hivyo hakuna fidia itakayotolewa isipokuwa tu kuacha huru Mtumwa Muislamu. Kwa nini fidia hapa haipo? Ni kwa sababu fidia kama itatolewa itakwenda kwa makafiri wenye uadui na Uislamu. Kuwapa fidia makafiri maadui ni kuwapa nguvu dhidi ya Waislamu.


3- - Pamoja na kwamba ndugu wa Muislamu aliyeuliwa ni makafiri lakini hapa Uislamu unawapa fidia kwa sababu fidia hiyo haitarajiwi kutumika katika kuwadhuru Waislamu kwa sababu makafiri hawa wamo katika mkataba wa kuishi kwa amani. Hapa tunajifunza namna Uislamu unavyothamini amani na utulivu katika jamii. Ndugu wa marehemu kama ni makafiri wasioingia mkataba wa amani na Waislamu hawapewi Dia. Ama kama ni makafiri walioingia mkataba wa amani na Waislamu wanapewa Dia kwa kuzingatia amani.


Sura: ANNISAI 

Aya : 114

۞لَّا خَيۡرَ فِي كَثِيرٖ مِّن نَّجۡوَىٰهُمۡ إِلَّا مَنۡ أَمَرَ بِصَدَقَةٍ أَوۡ مَعۡرُوفٍ أَوۡ إِصۡلَٰحِۭ بَيۡنَ ٱلنَّاسِۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٰلِكَ ٱبۡتِغَآءَ مَرۡضَاتِ ٱللَّهِ فَسَوۡفَ نُؤۡتِيهِ أَجۡرًا عَظِيمٗا

Hakuna kheri yoyote katika minong’ono yao mingi isipokuwa tu kwa yule anayeamrisha (kutoa) sadaka au (kutenda) jema au kupatanisha watu. Na yeyote atakayefanya hayo kwa kutaka radhi za Allah basi tutampa malipo makubwa kabisa



Sura: ATTAUBA 

Aya : 75

۞وَمِنۡهُم مَّنۡ عَٰهَدَ ٱللَّهَ لَئِنۡ ءَاتَىٰنَا مِن فَضۡلِهِۦ لَنَصَّدَّقَنَّ وَلَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na miongoni mwao (hao wanafiki) wapo waliomuahidi Allah kwamba: Iwapo (Allah) atatupa katika fadhila zake basi kwa yakini kabisa tutatoa sadaka sana na tutakuwa katika watendao mema



Sura: ATTAUBA 

Aya : 76

فَلَمَّآ ءَاتَىٰهُم مِّن فَضۡلِهِۦ بَخِلُواْ بِهِۦ وَتَوَلَّواْ وَّهُم مُّعۡرِضُونَ

Basi (Allah) alipowapa katika fadhila zake walizifanyia ubahili na wakakengeuka na huku wakipuuza (walichokiahidi)



Sura: ATTAUBA 

Aya : 77

فَأَعۡقَبَهُمۡ نِفَاقٗا فِي قُلُوبِهِمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ يَلۡقَوۡنَهُۥ بِمَآ أَخۡلَفُواْ ٱللَّهَ مَا وَعَدُوهُ وَبِمَا كَانُواْ يَكۡذِبُونَ

Basi (Allah) akawapa hatima ya unafiki nyoyoni mwao mpaka Siku watapokutana naye, kwa sababu ya kuwa walimhalifu Allah katika yale waliyomuahidi, na kwa sababu ya kusema kwao uwongo



Sura: ATTAUBA 

Aya : 103

خُذۡ مِنۡ أَمۡوَٰلِهِمۡ صَدَقَةٗ تُطَهِّرُهُمۡ وَتُزَكِّيهِم بِهَا وَصَلِّ عَلَيۡهِمۡۖ إِنَّ صَلَوٰتَكَ سَكَنٞ لَّهُمۡۗ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ

Chukua sadaka (Zaka) kutoka katika mali zao (waumini ili) uwasafishe na uwatakase kwazo na waombee rehema. Hakika dua yako ni (sababu ya) utuvu kwao. Na Allah ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua



Sura: ATTAUBA 

Aya : 104

أَلَمۡ يَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ هُوَ يَقۡبَلُ ٱلتَّوۡبَةَ عَنۡ عِبَادِهِۦ وَيَأۡخُذُ ٱلصَّدَقَٰتِ وَأَنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ

Je, (waumini na wanaotubu) hawajui ya kwamba Allah (ndiye) anayekubali Toba za waja wake, na anazikubali sadaka, na kwamba Allah tu ndiye Mwingi wa kupokea Toba, Rahimu sana?



Sura: AR-RA’D 

Aya : 22

وَٱلَّذِينَ صَبَرُواْ ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِمۡ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَأَنفَقُواْ مِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ سِرّٗا وَعَلَانِيَةٗ وَيَدۡرَءُونَ بِٱلۡحَسَنَةِ ٱلسَّيِّئَةَ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ عُقۡبَى ٱلدَّارِ

Na ambao husubiri kwa kutaka radhi za Mola wao Mlezi, na wakasimamisha Swala, na wakatoa katika tulivyowaruzuku kwa siri na kwa uwazi, na wakayaondoa maovu kwa mema. Hao ndio watakaopata malipo ya nyumba ya Akhera



Sura: IBRAHIM 

Aya : 31

قُل لِّعِبَادِيَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُنفِقُواْ مِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ سِرّٗا وَعَلَانِيَةٗ مِّن قَبۡلِ أَن يَأۡتِيَ يَوۡمٞ لَّا بَيۡعٞ فِيهِ وَلَا خِلَٰلٌ

Waambie waja wangu walioa-mini, wasimamishe Swala, na watoe katika tulivyowaruzuku, kwa siri na dhahiri, kabla haijafika Siku isiyofaa kitu fidia wala urafiki



Sura: AL-HAJJ 

Aya : 28

لِّيَشۡهَدُواْ مَنَٰفِعَ لَهُمۡ وَيَذۡكُرُواْ ٱسۡمَ ٱللَّهِ فِيٓ أَيَّامٖ مَّعۡلُومَٰتٍ عَلَىٰ مَا رَزَقَهُم مِّنۢ بَهِيمَةِ ٱلۡأَنۡعَٰمِۖ فَكُلُواْ مِنۡهَا وَأَطۡعِمُواْ ٱلۡبَآئِسَ ٱلۡفَقِيرَ

Ili washuhudie manufaa yao na walitaje jina la Allah katika siku maalumu juu ya wanyama hoa (wa kufugwa) alio waruzuku. Basi kuleni katika hao na mlisheni mwenye shida aliye fakiri



Sura: AL-HAJJ 

Aya : 36

وَٱلۡبُدۡنَ جَعَلۡنَٰهَا لَكُم مِّن شَعَـٰٓئِرِ ٱللَّهِ لَكُمۡ فِيهَا خَيۡرٞۖ فَٱذۡكُرُواْ ٱسۡمَ ٱللَّهِ عَلَيۡهَا صَوَآفَّۖ فَإِذَا وَجَبَتۡ جُنُوبُهَا فَكُلُواْ مِنۡهَا وَأَطۡعِمُواْ ٱلۡقَانِعَ وَٱلۡمُعۡتَرَّۚ كَذَٰلِكَ سَخَّرۡنَٰهَا لَكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ

Na ngamia wa sadaka tume-kufanyieni kuwa ni kudhihirisha matukuzo kwa Allah; kwa hao mna kheri nyingi. Basi litajeni jina la Allah juu yao wanapo simama kwa safu. Na waangukapo ubavu kuleni katika hao na walisheni walio kinai na wanao lazimika kuomba. Ndio kama hivi tumewafanya hawa wanyama dhalili kwenu ili mpate kushukuru



Sura: ARRUUM 

Aya : 39

وَمَآ ءَاتَيۡتُم مِّن رِّبٗا لِّيَرۡبُوَاْ فِيٓ أَمۡوَٰلِ ٱلنَّاسِ فَلَا يَرۡبُواْ عِندَ ٱللَّهِۖ وَمَآ ءَاتَيۡتُم مِّن زَكَوٰةٖ تُرِيدُونَ وَجۡهَ ٱللَّهِ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُضۡعِفُونَ

Allah ndiye aliye kuumbeni, kisha akakuruzukuni, kisha anakufisheni, na kisha anakufufueni. Je! Yupo yeyote katika hao mnao washirikisha na Allah afanyae lolote katika hayo? Yeye ametakasika, na ametukuka na hayo mnayo mshirikisha naye



Sura: SABAA 

Aya : 39

قُلۡ إِنَّ رَبِّي يَبۡسُطُ ٱلرِّزۡقَ لِمَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦ وَيَقۡدِرُ لَهُۥۚ وَمَآ أَنفَقۡتُم مِّن شَيۡءٖ فَهُوَ يُخۡلِفُهُۥۖ وَهُوَ خَيۡرُ ٱلرَّـٰزِقِينَ

Sema: Kwa hakika Mola wangu Mlezi humkunjulia riziki na humdhikisha amtakaye katika waja wake. Na chochote mtakacho kitoa Yeye atakilipa. Naye ni Mbora wa wanao ruzuku