Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 84

إِذۡ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلۡبٖ سَلِيمٍ

Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo ulio salama



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 85

إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَاذَا تَعۡبُدُونَ

Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 86

أَئِفۡكًا ءَالِهَةٗ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ

Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Allah?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 87

فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 88

فَنَظَرَ نَظۡرَةٗ فِي ٱلنُّجُومِ

Kisha akapiga jicho kutazama nyota



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 89

فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٞ

Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 90

فَتَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ مُدۡبِرِينَ

Nao wakamwacha, wakampa kisogo



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 91

فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمۡ فَقَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ

Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 92

مَا لَكُمۡ لَا تَنطِقُونَ

Mna nini hata hamsemi?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 93

فَرَاغَ عَلَيۡهِمۡ ضَرۡبَۢا بِٱلۡيَمِينِ

Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 94

فَأَقۡبَلُوٓاْ إِلَيۡهِ يَزِفُّونَ

Basi wakamjia upesi upesi



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 95

قَالَ أَتَعۡبُدُونَ مَا تَنۡحِتُونَ

Akasema: Hivyomnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 96

وَٱللَّهُ خَلَقَكُمۡ وَمَا تَعۡمَلُونَ

Na hali Allah ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 97

قَالُواْ ٱبۡنُواْ لَهُۥ بُنۡيَٰنٗا فَأَلۡقُوهُ فِي ٱلۡجَحِيمِ

Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 98

فَأَرَادُواْ بِهِۦ كَيۡدٗا فَجَعَلۡنَٰهُمُ ٱلۡأَسۡفَلِينَ

Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 99

وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهۡدِينِ

Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 100

رَبِّ هَبۡ لِي مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa wema



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 101

فَبَشَّرۡنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٖ

Basi tukambashiria mtoto aliye mpole



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 102

فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعۡيَ قَالَ يَٰبُنَيَّ إِنِّيٓ أَرَىٰ فِي ٱلۡمَنَامِ أَنِّيٓ أَذۡبَحُكَ فَٱنظُرۡ مَاذَا تَرَىٰۚ قَالَ يَـٰٓأَبَتِ ٱفۡعَلۡ مَا تُؤۡمَرُۖ سَتَجِدُنِيٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّـٰبِرِينَ

Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 103

فَلَمَّآ أَسۡلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلۡجَبِينِ

Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji (kifudifudi ili amchinje)



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 104

وَنَٰدَيۡنَٰهُ أَن يَـٰٓإِبۡرَٰهِيمُ

Tulimwita: Ewe Ibrahim!



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 105

قَدۡ صَدَّقۡتَ ٱلرُّءۡيَآۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 106

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡبَلَـٰٓؤُاْ ٱلۡمُبِينُ

Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 107

وَفَدَيۡنَٰهُ بِذِبۡحٍ عَظِيمٖ

Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu (mnyama wa kuchinja) mtukufu



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 108

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 109

سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ

Iwe salama kwa Ibrahim!



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 110

كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 111

إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 112

وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema



Sura: ASSWAAFFAAT 

Aya : 113

وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٞ وَظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٞ

Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa vizazi vyao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi