Sura: IBRAHIM 

Aya : 48

يَوۡمَ تُبَدَّلُ ٱلۡأَرۡضُ غَيۡرَ ٱلۡأَرۡضِ وَٱلسَّمَٰوَٰتُۖ وَبَرَزُواْ لِلَّهِ ٱلۡوَٰحِدِ ٱلۡقَهَّارِ

(Malipo yatakuwa) Siku itapogeuzwa ardhi iwe ardhi nyingine, na mbingu pia. Nao watahudhuria mbele ya Allah, Mwenye nguvu mno



Sura: AL-KAHF 

Aya : 47

وَيَوۡمَ نُسَيِّرُ ٱلۡجِبَالَ وَتَرَى ٱلۡأَرۡضَ بَارِزَةٗ وَحَشَرۡنَٰهُمۡ فَلَمۡ نُغَادِرۡ مِنۡهُمۡ أَحَدٗا

Na siku tutapo iondoa milima na ukaiona ardhi ipo wazi, na tukawafufua - wala hatutamwacha hata mmoja kati yao



Sura: MARYAM 

Aya : 40

إِنَّا نَحۡنُ نَرِثُ ٱلۡأَرۡضَ وَمَنۡ عَلَيۡهَا وَإِلَيۡنَا يُرۡجَعُونَ

Hakika Sisi tutairithi ardhi na walio juu yake. Na kwetu watare-jeshwa



Sura: TWAHA 

Aya : 105

وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡجِبَالِ فَقُلۡ يَنسِفُهَا رَبِّي نَسۡفٗا

Na wanakuuliza khabari za milima. Waambie: Mola wangu Mlezi ataivuruga vuruga



Sura: TWAHA 

Aya : 106

فَيَذَرُهَا قَاعٗا صَفۡصَفٗا

Aiache ardhi wakati huo ni tambarare, imelingana na imekuwa kavu haina mimea



Sura: TWAHA 

Aya : 107

لَّا تَرَىٰ فِيهَا عِوَجٗا وَلَآ أَمۡتٗا

Hutaona humo mdidimio wala muinuko



Sura: AL-HAJJ 

Aya : 65

أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ سَخَّرَ لَكُم مَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَٱلۡفُلۡكَ تَجۡرِي فِي ٱلۡبَحۡرِ بِأَمۡرِهِۦ وَيُمۡسِكُ ٱلسَّمَآءَ أَن تَقَعَ عَلَى ٱلۡأَرۡضِ إِلَّا بِإِذۡنِهِۦٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ بِٱلنَّاسِ لَرَءُوفٞ رَّحِيمٞ

Je! Huoni kwamba Allah amevidhalilisha kwenu viliomo katika ardhi, na marikebu zipitazo baharini kwa amri yake, na amezishika mbingu zisianguke juu ya ardhi ila kwa idhini yake. Hakika Allah ni Mwenye huruma kwa watu, Mwenye kurehemu



Sura: ANNAMLI 

Aya : 88

وَتَرَى ٱلۡجِبَالَ تَحۡسَبُهَا جَامِدَةٗ وَهِيَ تَمُرُّ مَرَّ ٱلسَّحَابِۚ صُنۡعَ ٱللَّهِ ٱلَّذِيٓ أَتۡقَنَ كُلَّ شَيۡءٍۚ إِنَّهُۥ خَبِيرُۢ بِمَا تَفۡعَلُونَ

Na unaiona milima unaidhania imetulia; nayo inakwenda kama mwendo wa mawingu. Huo ndio ufundi wa Allah aliye tengeneza kila kitu kwa ubora. Hakika Yeye anazo khabari za yote myatendayo



Sura: AZZUMAR 

Aya : 67

وَمَا قَدَرُواْ ٱللَّهَ حَقَّ قَدۡرِهِۦ وَٱلۡأَرۡضُ جَمِيعٗا قَبۡضَتُهُۥ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ وَٱلسَّمَٰوَٰتُ مَطۡوِيَّـٰتُۢ بِيَمِينِهِۦۚ سُبۡحَٰنَهُۥ وَتَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Na wala hawakumheshimu Allah kama anavyo stahiki kadiri yake. Na Siku ya Kiyama ardhi yote itakuwa mkononi mwake, na mbingu zitakunjwa katika mkono wake wa kuume. Subhanahu wa Taa’la Ametakasika na Ametukuka na hayo wanayo mshirikisha nayo



Sura: AZZUMAR 

Aya : 68

وَنُفِخَ فِي ٱلصُّورِ فَصَعِقَ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ إِلَّا مَن شَآءَ ٱللَّهُۖ ثُمَّ نُفِخَ فِيهِ أُخۡرَىٰ فَإِذَا هُمۡ قِيَامٞ يَنظُرُونَ

Na litapulizwa barugumu, wazimie (wafe) waliomo mbinguni na waliomo katika ardhi, isipo kuwa aliye mtaka Allah. Kisha litapulizwa mara nyengine. Hapo watainuka wawe wanangojea



Sura: AZZUMAR 

Aya : 69

وَأَشۡرَقَتِ ٱلۡأَرۡضُ بِنُورِ رَبِّهَا وَوُضِعَ ٱلۡكِتَٰبُ وَجِاْيٓءَ بِٱلنَّبِيِّـۧنَ وَٱلشُّهَدَآءِ وَقُضِيَ بَيۡنَهُم بِٱلۡحَقِّ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na ardhi itang’ara kwa Nuru ya Mola wake Mlezi, na Kitabu kitawekwa, na wataletwa Manabii na mashahidi, na patahukumiwa baina yao kwa haki, wala hawata-dhulumiwa



Sura: QAAF 

Aya : 44

يَوۡمَ تَشَقَّقُ ٱلۡأَرۡضُ عَنۡهُمۡ سِرَاعٗاۚ ذَٰلِكَ حَشۡرٌ عَلَيۡنَا يَسِيرٞ

Siku itakayowapasukia ardhi (watoke) haraka haraka. Huo ndio mkusanyo, ni mwepesi kabisa kwetu



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 4

إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا

Wakati ardhi itakapotikiswa mtikiso mkubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 5

وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا

Na milima ikapondwa pondwa upondwaji mkubwa



Sura: AL-WAAQIA’H 

Aya : 6

فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا

(Kwa sababu ya kupondwa pondwa huko, milima) ikawa vumbi lenye kutawanyika



Sura: ALHAAQQA 

Aya : 14

وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ

Na ardhi na majabali ikaondolewa kisha ika pondwa pondwa mpondo mmoja



Sura: ALMUZZAMMIL 

Aya : 14

يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ وَكَانَتِ ٱلۡجِبَالُ كَثِيبٗا مَّهِيلًا

Siku ambayo ardhi itatikisika na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga



Sura: ANNABAI 

Aya : 20

وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا

Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi, [mangati]



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 3

وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ

Na ardhi itakapo tanuliwa,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 4

وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ

Na kuvitoa vilivyokuwa ndani yake, ikawa tupu,



Sura: AL-INSHIQAAQ 

Aya : 5

وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapaswa kumsikiliza,



Sura: AL-FAJRI 

Aya : 21

كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 1

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا

Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 2

وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا

Na itakapo toa ardhi mizigo yake!



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 3

وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا

Na mtu akasema: Ina nini?



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 4

يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا

Siku hiyo itahadithia khabari zake



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 5

بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا

Kwasababu Mola wake Mlezi ameifunulia!