Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 17

سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا

Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 18

إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ

Kwani hakika yeye alifikiri na akapima



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 19

فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Basi ameangamia! Namna alivyo pima



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 20

ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ

Tena ameangamia! Namna alivyo pima!



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 21

ثُمَّ نَظَرَ

Kisha akatazama



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 22

ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ

Kisha akakunja paji (la uso) na akafinya uso kwa ghadhabu



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 23

ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ

Kisha akageuka nyuma, na akaipa kisogo haki, na akatakabari



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 24

فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ

Na akasema: Hii (Qurani) si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 25

إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ

Hii si chochote isipokuwa ni kauli ya binadamu



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 26

سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ

Nitamuingiza (na kumuunguza) kwenye Moto wa saqar



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 27

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ

Na ni nini kitakujuulisha nini huo Moto wa Saqar?



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 28

لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ

Haubakishi wala hauachi, (kitu chochote)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 29

لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ

Wenye kubabua vikali ngozi, (iwe nyeusi)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 30

عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ

Juu yake wako (walinzi) kumi na tisa



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 31

وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَـٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ

Na Hatukuweka walinzi wa moto isipokuwa ni Malaika, na Hatukufanya idadi yao isipokuwa iwe ni mtihani kwa wale waliokufuru; ili wawe na yakini wale waliopewa Kitabu, na iwazidishie Imani wale walioamini; na wala wasitie shaka wale waliopewa Kitabu na Waumini; na ili wale waliokuwa na maradhi nyoyoni mwao (ya unafiki), na makafiri waseme: Allah Amekusudia nini kwa mfano huu? Hivyo ndivyo Allah Anavyompoteza Amtakaye na Anamuongoa Amtakaye. Na hakuna ajuaye majeshi ya Mola wako isipokuwa Yeye Peke yake, na haya hayakuwa isipokuwa ni ukumbusho tu kwa binadamu



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 32

كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ

Sivyo hivyo! Naapa kwa mwezi



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 33

وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ

Na Naapa kwa usiku unapoondoka



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 34

وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ

Na Naapa kwa asubuhi inapoangaza (inapo pambazuka)



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 35

إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ

Hakika huo (Moto) bila shaka ni mojawapo ya majanga makubwa kabisa



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 36

نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ

Ni onyo kwa binadamu



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 37

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ

Kwa atakaye miongoni mwenu atatangulia mbele au atachelewa nyuma



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 38

كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ

Kila nafsi iko katika rehani kwa yale iliyoyachuma.[1]


1- - Kila nafsi itashikwa kwa iliyo yatenda.


Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 39

إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ

Isipokuwa watu wa kuliani



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 40

فِي جَنَّـٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ

Hao watakuwa katika Mabustani ya Peponi, wanaulizana



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 41

عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Kuhusu wakosefu



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 42

مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ

(Watawauliza): Nini kilicho kuingizeni katika Moto?



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 43

قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ

Watasema: Hatukuwa miongoni mwa wanaosali



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 44

وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ

Na wala hatukuwa tunalisha masikini



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 45

وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ

Na tulikuwa tukipiga porojo pamoja na wanaopiga porojo



Sura: ALMUDDATH-THIR 

Aya : 46

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na tulikuwa tunaikadhibisha Siku ya malipo