Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 17

فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ

Basi na awaite wenzake!



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 18

سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ

Nasi tutawaita Mazabania!



Sura: AL-A’LAQ 

Aya : 19

كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩

Hasha! Usimtii! Nawe sujudu na ujongee!



Sura: AL-QADRI 

Aya : 1

إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ فِي لَيۡلَةِ ٱلۡقَدۡرِ

Hakika Sisi tumeiteremsha (Qur’ani) katika Laylatul Qadri (Usikuwa mtukufu wenye Cheo)



Sura: AL-QADRI 

Aya : 2

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ

Na nini kitakacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?



Sura: AL-QADRI 

Aya : 3

لَيۡلَةُ ٱلۡقَدۡرِ خَيۡرٞ مِّنۡ أَلۡفِ شَهۡرٖ

Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu



Sura: AL-QADRI 

Aya : 4

تَنَزَّلُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ فِيهَا بِإِذۡنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمۡرٖ

Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo



Sura: AL-QADRI 

Aya : 5

سَلَٰمٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطۡلَعِ ٱلۡفَجۡرِ

(Ni) amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 1

لَمۡ يَكُنِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ مُنفَكِّينَ حَتَّىٰ تَأۡتِيَهُمُ ٱلۡبَيِّنَةُ

Hawakuwa walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina (makafiri) waache walio nayo mpaka iwajie bayana,



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 2

رَسُولٞ مِّنَ ٱللَّهِ يَتۡلُواْ صُحُفٗا مُّطَهَّرَةٗ

Yaani Mtume aliyetoka kwa Allah anaye wasomea kurasa zilizo takasika,



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 3

فِيهَا كُتُبٞ قَيِّمَةٞ

Ndani yake mna maandiko yaliyo nyooka



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 4

وَمَا تَفَرَّقَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَةُ

Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 5

وَمَآ أُمِرُوٓاْ إِلَّا لِيَعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَ حُنَفَآءَ وَيُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَيُؤۡتُواْ ٱلزَّكَوٰةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ ٱلۡقَيِّمَةِ

Nao hawakuamrishwa kitu isipokuwa wamuabudu Allah kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 6

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمۡ شَرُّ ٱلۡبَرِيَّةِ

Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 7

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمۡ خَيۡرُ ٱلۡبَرِيَّةِ

Hakika walio amini na wakatenda mema, hao ndio bora wa viumbe



Sura: AL-BAYYINAH 

Aya : 8

جَزَآؤُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتُ عَدۡنٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ ذَٰلِكَ لِمَنۡ خَشِيَ رَبَّهُۥ

Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za daima, zipitazo mito kati yake. Wakae humo milele. Allah yupo radhi nao, na wao waporadhi naye. Hayo ni kwa anaye muogopa Mola wake Mlezi



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 1

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا

Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 2

وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا

Na itakapo toa ardhi mizigo yake!



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 3

وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا

Na mtu akasema: Ina nini?



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 4

يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا

Siku hiyo itahadithia khabari zake



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 5

بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا

Kwasababu Mola wake Mlezi ameifunulia!



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 6

يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ

Siku hiyo watu watatoka wakiwa tofauti tofauti wakaonyweshwe vitendo vyao!



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 7

فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ

Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!



Sura: AZZILZAAL 

Aya : 8

وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ

Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!



Sura: AL-AADIYAAT 

Aya : 1

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا

Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,



Sura: AL-AADIYAAT 

Aya : 2

فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا

Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,



Sura: AL-AADIYAAT 

Aya : 3

فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا

Wakishambulia wakati wa asubuhi,



Sura: AL-AADIYAAT 

Aya : 4

فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا

Huku wakitimua vumbi,



Sura: AL-AADIYAAT 

Aya : 5

فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا

Na wakijitoma kati ya kundi,



Sura: AL-AADIYAAT 

Aya : 6

إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ

Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!