Sura: AL-KAAFIRUUN 

Aya : 6

لَكُمۡ دِينُكُمۡ وَلِيَ دِينِ

Nyinyi mna dini yenu, nami nina dini yangu



Sura: ANASRI 

Aya : 1

إِذَا جَآءَ نَصۡرُ ٱللَّهِ وَٱلۡفَتۡحُ

Itakapokuja nusra ya Allah na ushindi (ukombozi wa mji wa Makka)



Sura: ANASRI 

Aya : 2

وَرَأَيۡتَ ٱلنَّاسَ يَدۡخُلُونَ فِي دِينِ ٱللَّهِ أَفۡوَاجٗا

Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Allah kwa makundi



Sura: ANASRI 

Aya : 3

فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَٱسۡتَغۡفِرۡهُۚ إِنَّهُۥ كَانَ تَوَّابَۢا

Basi zitakase sifa za Mola wako Mlezi na muombe msamaha. Hakika, Yeye (Allah) amekuwa Mwenye kukubali sana toba. Sura imetoa utabiri wa kifo cha Mtume rehma na amani ziwe juu yake



Sura: AL-MASAD

Aya : 1

تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ

Imeangamia mikono ya Abulahab na yeye (kwa maana hiyo) ameangamia



Sura: AL-MASAD

Aya : 2

مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ

Haitamfaa mali yake na (vitendo) alivyovichuma (alivyovifanya)



Sura: AL-MASAD

Aya : 3

سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ

Atauingia moto wenye muwako



Sura: AL-MASAD

Aya : 4

وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ

(Ataingia Motoni yeye) Na mkewe, mchukuzi mkubwa wa kuni



Sura: AL-MASAD

Aya : 5

فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ

Shingoni mwake iko kamba ya kusokotwa



Sura: AL-IKHLAAS 

Aya : 1

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ

Sema: Yeye Allah ni wa pekee



Sura: AL-IKHLAAS 

Aya : 2

ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ

Allah ndiye tu Mkusudiwa (katika kuabudiwa, kutegemewa na kutatua shida za watu)



Sura: AL-IKHLAAS 

Aya : 3

لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ

Hakuzaa[1] na hakuzaliwa.[2]


1- - Kwa maana hiyo hana mtoto.


2- - Kwa maana hiyo hana baba wala mama.

---------------

------------------------------------------------------------

---------------

------------------------------------------------------------


Sura: AL-IKHLAAS 

Aya : 4

وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدُۢ

Na hakuna yeyote anaye fanana naye



Sura: AL-FALAQ

Aya : 1

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ

Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko



Sura: AL-FALAQ

Aya : 2

مِن شَرِّ مَا خَلَقَ

(Najikinga) Dhidi ya shari ya alivyoviumba



Sura: AL-FALAQ

Aya : 3

وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya giza la usiku liingiapo



Sura: AL-FALAQ

Aya : 4

وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّـٰثَٰتِ فِي ٱلۡعُقَدِ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya (wanawake) wanaopulizia mafundoni



Sura: AL-FALAQ

Aya : 5

وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya hasidi anapo husudu



Sura: ANNAAS

Aya : 1

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ

Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa watu



Sura: ANNAAS

Aya : 2

مَلِكِ ٱلنَّاسِ

Mfalme wa watu



Sura: ANNAAS

Aya : 3

إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ

Muabudiwa wa haki wa watu (Mwenye haki ya kuabudiwa na watu)



Sura: ANNAAS

Aya : 4

مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ

(Najilinda dhidi ya shari ya (shetani) mwenye kutia wasiwasi, mwenye kurejea nyuma



Sura: ANNAAS

Aya : 5

ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ

Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu



Sura: ANNAAS

Aya : 6

مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ

(Shetani) Anayetokana na majini na watu