Sura: ANNAJMI 

Aya : 12

أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ

Je, mnambishia kuhusu yale aliyoyaona?



Sura: ANNAJMI 

Aya : 13

وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ

Na hakika alimuona (Jibriyl) kwa mara nyingine



Sura: ANNAJMI 

Aya : 14

عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Kwenye mkunazi wa mpaka wa mwisho kabisa



Sura: ANNAJMI 

Aya : 15

عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ

Karibu yake kuna Jannatu Al-Ma-waa



Sura: ANNAJMI 

Aya : 16

إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ

Ulipoufunika mkunazi huo hicho kilicho ufinika



Sura: ANNAJMI 

Aya : 17

مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ

Jicho lake halikukengeuka wala halikupindukia mipaka



Sura: ANNAJMI 

Aya : 18

لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ

Kwa yakini aliona miongoni mwa Aayaat (ishara, dalili) za Bwana wake kubwa kabisa



Sura: ANNAJMI 

Aya : 19

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّـٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ

Je, mmeona (masanamu) Laata na ‘Uzzaa?



Sura: ANNAJMI 

Aya : 20

وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ

Na Manaata mwengine wa tatu?



Sura: ANNAJMI 

Aya : 21

أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ

Je, nyinyi mna wana wa kiume Naye Ana wana wa kike?



Sura: ANNAJMI 

Aya : 22

تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ

Huo basi ni mgao wa dhulma!



Sura: ANNAJMI 

Aya : 23

إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ

Hayo si chochote isipokuwa ni majina mmeyaita nyinyi na baba zenu, wala Allah Hakuyateremshia dalili yoyote. Hawafuati isipokuwa dhana na yale yanayotamani nafsi (zao), na hali imekwishawajia kutoka kwa Bwana wao mwongozo



Sura: ANNAJMI 

Aya : 24

أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ

Kwani kila Mtu anapata kila anayoyatamani?



Sura: ANNAJMI 

Aya : 25

فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ

Na Allah ndiye mmiliki wa Akhera na Dunia



Sura: ANNAJMI 

Aya : 26

۞وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ

Na kuna malaika wengi mbinguni hainufaishi chochote uombezi wao ila baada ya kupewa idhini na Allah kwa amtakaye na amridhie



Sura: ANNAJMI 

Aya : 27

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ

Hakika wale wasioamini Aakhirah bila shaka wanawaita Malaika kwa majina ya kike



Sura: ANNAJMI 

Aya : 28

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا

Na wala hawana ujuzi wowote ule wa hayo; hawafuati isipokuwa dhana, na hakika dhana haifai kitu chochote mbele ya haki



Sura: ANNAJMI 

Aya : 29

فَأَعۡرِضۡ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكۡرِنَا وَلَمۡ يُرِدۡ إِلَّا ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Basi achana naye ambaye ameupa mgongo ukumbusho Wetu na wala hataki isipokuwa maisha ya dunia



Sura: ANNAJMI 

Aya : 30

ذَٰلِكَ مَبۡلَغُهُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱهۡتَدَىٰ

Huo ndio upeo wao wa elimu. Hakika Bwana wako ni Mjuzi zaidi wa ambaye amepotoka njia Yake, Naye Mjuzi zaidi wa ambaye ameongoka



Sura: ANNAJMI 

Aya : 31

وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ لِيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَسَـٰٓـُٔواْ بِمَا عَمِلُواْ وَيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ بِٱلۡحُسۡنَى

Na ni vya Allah Pekee vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini, ili Awalipe wale waliofanya uovu kwa yale waliyoyatenda, na Awalipe wale waliofanya mema kwa mema zaidi



Sura: ANNAJMI 

Aya : 32

ٱلَّذِينَ يَجۡتَنِبُونَ كَبَـٰٓئِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلۡمَغۡفِرَةِۚ هُوَ أَعۡلَمُ بِكُمۡ إِذۡ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَإِذۡ أَنتُمۡ أَجِنَّةٞ فِي بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمۡۖ فَلَا تُزَكُّوٓاْ أَنفُسَكُمۡۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ

Wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na machafu isipokuwa makosa madogo-madogo. Hakika Bwana wako ni Mwingi wa msamaha. Yeye Anakujueni vyema, tangu Alipokuanzisheni kutoka katika ardhi, na pale mlipokuwa mimba changa matumboni mwa mama zenu. Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa



Sura: ANNAJMI 

Aya : 33

أَفَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي تَوَلَّىٰ

Hivi umemuona yule ambaye amekengeuka



Sura: ANNAJMI 

Aya : 34

وَأَعۡطَىٰ قَلِيلٗا وَأَكۡدَىٰٓ

Na Akatoa kidogo, kisha akazuia.?



Sura: ANNAJMI 

Aya : 35

أَعِندَهُۥ عِلۡمُ ٱلۡغَيۡبِ فَهُوَ يَرَىٰٓ

hivi yeye ana elimu ya ghaibu basi kwa elimu hiyo yeye anaona?



Sura: ANNAJMI 

Aya : 36

أَمۡ لَمۡ يُنَبَّأۡ بِمَا فِي صُحُفِ مُوسَىٰ

Au hawajaambiwa kwa ambayo yamo kwenye kitabu cha Mussa?



Sura: ANNAJMI 

Aya : 37

وَإِبۡرَٰهِيمَ ٱلَّذِي وَفَّىٰٓ

Na Ibraahim aliyetimiza (ahadi)



Sura: ANNAJMI 

Aya : 38

أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰ

Na kwamba mbebaji dhambi hatobeba mzigo wa mwengine



Sura: ANNAJMI 

Aya : 39

وَأَن لَّيۡسَ لِلۡإِنسَٰنِ إِلَّا مَا سَعَىٰ

Na kwamba Mtu hatopata malipo isipokuwa yale aliyoyafanyia juhudi



Sura: ANNAJMI 

Aya : 40

وَأَنَّ سَعۡيَهُۥ سَوۡفَ يُرَىٰ

Na kwamba juhudi yake itakuja kuonekana



Sura: ANNAJMI 

Aya : 41

ثُمَّ يُجۡزَىٰهُ ٱلۡجَزَآءَ ٱلۡأَوۡفَىٰ

Kisha atalipwa malipo yake kamilifu