Sura: AL-IMRAN 

Aya : 87

أُوْلَـٰٓئِكَ جَزَآؤُهُمۡ أَنَّ عَلَيۡهِمۡ لَعۡنَةَ ٱللَّهِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ وَٱلنَّاسِ أَجۡمَعِينَ

Hao malipo yao ni kwamba, watashukiwa na laana ya Allah na ya Malaika na ya watu wote



Sura: AL-IMRAN 

Aya : 88

خَٰلِدِينَ فِيهَا لَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابُ وَلَا هُمۡ يُنظَرُونَ

Watabaki milele humo (kwenye laana); hawatapunguziwa adhabu na hawatangojwa (hawatapewa muda wa kujitetea au kuomba msamaha)



Sura: AL-IMRAN 

Aya : 89

إِلَّا ٱلَّذِينَ تَابُواْ مِنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ وَأَصۡلَحُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ

Isipokuwa (watakaoepuka laana ni) wale waliotubu baada ya hapo na wakafanya mema. Basi kwa hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno



Sura: AL-IMRAN 

Aya : 90

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بَعۡدَ إِيمَٰنِهِمۡ ثُمَّ ٱزۡدَادُواْ كُفۡرٗا لَّن تُقۡبَلَ تَوۡبَتُهُمۡ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلضَّآلُّونَ

Hakika, wale waliokufuru baada ya kuamini kisha wakazidisha ukafiri, toba zao hazitakubaliwa, na hao ndio hasa wapotevu



Sura: AL-IMRAN 

Aya : 91

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَمَاتُواْ وَهُمۡ كُفَّارٞ فَلَن يُقۡبَلَ مِنۡ أَحَدِهِم مِّلۡءُ ٱلۡأَرۡضِ ذَهَبٗا وَلَوِ ٱفۡتَدَىٰ بِهِۦٓۗ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ وَمَا لَهُم مِّن نَّـٰصِرِينَ

Hakika, wale waliokufuru na wakafa wakiwa makafiri, kamwe hatakubaliwa mmoja wao hata kama atajikomboa kwa kutoa fidia ya dhahabu ujazo wa ardhi yote. Hao watapata adhabu yenye maumivu makali mno na hawatakuwa na watetezi (wowote)



Sura: AL-IMRAN 

Aya : 92

لَن تَنَالُواْ ٱلۡبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُواْ مِمَّا تُحِبُّونَۚ وَمَا تُنفِقُواْ مِن شَيۡءٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٞ

Hamtaupata wema hadi mtoe katika mnavyovipenda. Na kitu chochote mtakachokitoa, hakika Allah anakijua sana