Sura: QAAF 

Aya : 31

وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ غَيۡرَ بَعِيدٍ

Na Pepo italetwa karibu kwa kwaajili ya Wacha Mungu, haitakuwa mbali



Sura: QAAF 

Aya : 32

هَٰذَا مَا تُوعَدُونَ لِكُلِّ أَوَّابٍ حَفِيظٖ

(Itasemwa): Haya ndiyo yale mliyoahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Allah, kwa kutubia, mwenye kuhifadhi vyema (amri za Allah)



Sura: QAAF 

Aya : 33

مَّنۡ خَشِيَ ٱلرَّحۡمَٰنَ بِٱلۡغَيۡبِ وَجَآءَ بِقَلۡبٖ مُّنِيبٍ

Anayemuogopa Allah (Mwingi wa Rehema) hali yakuwa hamuoni akaja na moyo ulioelekea kwake



Sura: QAAF 

Aya : 34

ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٖۖ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡخُلُودِ

Ingieni kwa amani hiyo ndiyo siku ya kukaa milele



Sura: QAAF 

Aya : 35

لَهُم مَّا يَشَآءُونَ فِيهَا وَلَدَيۡنَا مَزِيدٞ

Humo watakuwa na kila wanachokitaka na kwetu sisi kuna ziada. (ya kumuona Allah)



Sura: QAAF 

Aya : 36

وَكَمۡ أَهۡلَكۡنَا قَبۡلَهُم مِّن قَرۡنٍ هُمۡ أَشَدُّ مِنۡهُم بَطۡشٗا فَنَقَّبُواْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ هَلۡ مِن مَّحِيصٍ

Na Watu wa karne ngapi Tumewaaangamiza kabla yao ambao walikuwa wenye nguvu zaidi kuliko wao. Basi walitangatanga sana katika nchi nyingi. Je, kuna mahali popote pa kukimbilia?



Sura: QAAF 

Aya : 37

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَذِكۡرَىٰ لِمَن كَانَ لَهُۥ قَلۡبٌ أَوۡ أَلۡقَى ٱلسَّمۡعَ وَهُوَ شَهِيدٞ

Hakika katika hayo kuna ukumbusho kwa mtu mwenye moyo au ametega sikio nae yupo anashuhudia



Sura: QAAF 

Aya : 38

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ وَمَا مَسَّنَا مِن لُّغُوبٖ

Na kwa yakini Tumeumba mbingu na ardhi na vilivyo baina yake katika siku sita, na wala Hauku-tugusa uchovu wowote



Sura: QAAF 

Aya : 39

فَٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ قَبۡلَ طُلُوعِ ٱلشَّمۡسِ وَقَبۡلَ ٱلۡغُرُوبِ

Basi vumilia kwa hayo wanayoyasema na mtakase Mola wako kwa kumhimidi kabla kuchomoza jua na kabla ya kuchwa



Sura: QAAF 

Aya : 40

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَأَدۡبَٰرَ ٱلسُّجُودِ

Na katika majira ya usiku pia mtakase yeye na baada ya kusujudu



Sura: QAAF 

Aya : 41

وَٱسۡتَمِعۡ يَوۡمَ يُنَادِ ٱلۡمُنَادِ مِن مَّكَانٖ قَرِيبٖ

Na sikiliza kwa makini Siku atakayonadi mwenye kunadi kutoka mahali pa karibu



Sura: QAAF 

Aya : 42

يَوۡمَ يَسۡمَعُونَ ٱلصَّيۡحَةَ بِٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡخُرُوجِ

Siku watakayosikia ukelele kwa haki. Hiyo ndio Siku ya kutoka (makaburini na kufufuka)



Sura: QAAF 

Aya : 43

إِنَّا نَحۡنُ نُحۡيِۦ وَنُمِيتُ وَإِلَيۡنَا ٱلۡمَصِيرُ

Hakika sisi ndiyo tunaohuisha na tunafisha na kwetu sisi tu ndiyo marejeo



Sura: QAAF 

Aya : 44

يَوۡمَ تَشَقَّقُ ٱلۡأَرۡضُ عَنۡهُمۡ سِرَاعٗاۚ ذَٰلِكَ حَشۡرٌ عَلَيۡنَا يَسِيرٞ

Siku itakayowapasukia ardhi (watoke) haraka haraka. Huo ndio mkusanyo, ni mwepesi kabisa kwetu



Sura: QAAF 

Aya : 45

نَّحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَا يَقُولُونَۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡهِم بِجَبَّارٖۖ فَذَكِّرۡ بِٱلۡقُرۡءَانِ مَن يَخَافُ وَعِيدِ

Sisi tunayajua wanayoyasema na wewe hukuwa mwenye kuwatenza nguvu, basi wakumbushe kwa Qur’ani yeyote mwenye kuogopa onyo langu



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 1

وَٱلذَّـٰرِيَٰتِ ذَرۡوٗا

Ninaapa kwa upepo (mkali) unaopeperusha (kila kitu)



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 2

فَٱلۡحَٰمِلَٰتِ وِقۡرٗا

Kisha (ninaapa) wa vile vibebavyo uzito (ikiwa ni pamoja na mawingu yanayobeba maji ya mvua)



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 3

فَٱلۡجَٰرِيَٰتِ يُسۡرٗا

Kisha (ninaapa) kwa (majahazi na vyombo vingine vizito vya majini) yenye kutembea (juu ya maji) kwa wepesi



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 4

فَٱلۡمُقَسِّمَٰتِ أَمۡرًا

Kisha (ninaapa) kwa (Malaika) wanaogawa mambo (majukumu waliyopewa na Allah)



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 5

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٞ

(Kwamba) Hakika ilivyo ni kwamba, mnachoahidiwa ni kweli kabisa



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 6

وَإِنَّ ٱلدِّينَ لَوَٰقِعٞ

Na Hakika, malipo (Siku ya Kiyama) kwa yakini kabisa yatakuwepo



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 7

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡحُبُكِ

Nina apa kwa mbingu yenye njia



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 8

إِنَّكُمۡ لَفِي قَوۡلٖ مُّخۡتَلِفٖ

(Kwamba) Hakika, nyinyi mmo katika zinazotofautiana.[1]


1- - Mara mseme Muhammad ni muongo, mara mchawi n.k.


Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 9

يُؤۡفَكُ عَنۡهُ مَنۡ أُفِكَ

Huondolewa Humo Yule Anaye-ondolewa



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 10

قُتِلَ ٱلۡخَرَّـٰصُونَ

Wamelaaniwa Wakadhibishaji



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 11

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي غَمۡرَةٖ سَاهُونَ

Wale Ambao Wamezama Katika Ujinga Hali Ya Kujisahau



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 12

يَسۡـَٔلُونَ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Wanauliza Ni Lini Hiyo Siku Ya Malipo



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 13

يَوۡمَ هُمۡ عَلَى ٱلنَّارِ يُفۡتَنُونَ

Siku Hiyo Wao Katika Moto Watachomwa



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 14

ذُوقُواْ فِتۡنَتَكُمۡ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تَسۡتَعۡجِلُونَ

Onjeni Adhabu Yenu Hii Ambayo Mlikua Kwayo Mnaiharakisha



Sura: ADH-DHAARIYAAT 

Aya : 15

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٍ

Hakika Ya Wachamungu Watakua Ndani Ya Pepo Na Chemchem